-
Jifunze na Uwafundishe Wengine Maadili ya KikristoMnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
-
-
13. (a) Biblia inatusaidiaje kuhusiana na maadili? (b) Onyesha jambo kuu katika ushauri uliotolewa kwenye 1 Wathesalonike 4:3-7.
13 Maadili huathiri watu wengine pia. Kuna mifano katika Neno la Mungu inayoonyesha manufaa ya kufuata viwango vya Mungu vya maadili na matokeo ya kuvipuuza. (Mwanzo 39:1-9, 21; Yoshua 7:1-25) Unaweza pia kupata ushauri ulio wazi kuhusu maadili kama huu: “Haya ndiyo mapenzi ya Mungu, kule kutakaswa kwenu, kwamba mjiepushe na uasherati; kwamba kila mmoja wenu apaswe kujua jinsi ya kupata umiliki wa chombo chake mwenyewe katika utakaso na heshima, si katika hamu yenye tamaa ya ngono kama ile waliyo nayo pia mataifa wale wasiomjua Mungu; kwamba yeyote asifikie hatua ya kudhuru na kuziingilia haki za ndugu yake katika jambo hilo, . . . kwa maana Mungu alituita sisi, si kwa kuruhusu ukosefu wa usafi, bali kwa kuhusiana na utakaso.”—1 Wathesalonike 4:3-7.
14. Unaweza kujiuliza maswali gani kuhusiana na ushauri kwenye andiko la 1 Wathesalonike 4:3-7?
14 Andiko hilo linaonyesha wazi kwamba mwenendo mchafu kingono huvunja maadili ya Kikristo. Hata hivyo, unaweza kuelewa andiko hilo kwa undani zaidi. Maandiko fulani yana mambo mengi tunayoweza kujifunza na kutafakari, na hivyo kuyafahamu kwa undani na kwa usahihi zaidi. Kwa mfano, unaweza kutafakari juu ya yale ambayo Paulo alimaanisha aliposema kwamba kufanya uasherati kunaweza kufanya mtu ‘afikie hatua ya kudhuru na kuziingilia haki za ndugu yake katika jambo hilo.’ Ni haki gani zinazotajwa, na kuelewa jambo hilo vema kunaweza kukuchocheaje zaidi udumishe maadili ya Kikristo? Matokeo ya utafiti huo yanaweza kukusaidiaje uwafundishe wengine na kuwasaidia wamheshimu Mungu?
-
-
Jifunze na Uwafundishe Wengine Maadili ya KikristoMnara wa Mlinzi—2002 | Juni 15
-
-
16, 17. (a) Unaweza kupata wapi ufafanuzi kuhusu haki zilizotajwa kwenye andiko la 1 Wathesalonike 4:6? (b) Uasherati unaweza kuingilia haki za wengine katika njia zipi?
16 Hebu tufikirie mfano uliotajwa juu kwenye andiko la 1 Wathesalonike 4:3-7. Suala lilitokea kuhusu haki. Haki za nani? Nazo haki hizo zinaweza kuingiliwa jinsi gani? Kwa kutumia vifaa vya kujifunzia vilivyotajwa, unaweza kupata maelezo yanayofafanua mistari hiyo, kutia ndani haki ambazo Paulo alitaja. Unaweza kusoma maelezo hayo katika Insight on the Scriptures, Buku la Kwanza, ukurasa wa 863-864; Amani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?, ukurasa wa 145; gazeti Mnara wa Mlinzi la Novemba 15, 1989, ukurasa wa 31.
17 Ukiendelea kujifunza, utaona kwamba vichapo hivyo vinathibitisha yale ambayo Paulo alisema. Mwasherati humtenda Mungu dhambi na kujiweka katika hatari ya kupatwa na magonjwa. (1 Wakorintho 6:18, 19; Waebrania 13:4) Mwanamume anayefanya uasherati na mwanamke, huingilia haki za mwanamke huyo. Yeye huchafua maadili na dhamiri ya mwanamke huyo. Ikiwa hajaolewa, haki yake ya kufunga ndoa akiwa bikira huvunjwa, naye mtu atakayemwoa hunyimwa haki ya kufunga ndoa na bikira. Mwanamume huyo huwaumiza wazazi na mume wa mwanamke huyo ikiwa ameolewa. Mwanamume huyo asiye na maadili huinyima familia yake haki ya kuwa na sifa nzuri kiadili. Ikiwa yeye ni mshiriki wa kutaniko la Kikristo, analiaibisha na kuliharibia sifa kutaniko.—1 Wakorintho 5:1.
18. Unafaidikaje na funzo la Biblia kuhusu maadili ya Kikristo?
18 Maelezo hayo kuhusu haki yanakusaidia kuelewa kindani zaidi mstari huo. Bila shaka, ukiendelea kujifunza kwa njia hiyo utaelewa Maandiko vizuri zaidi na utanufaika sana. Ufahamu wako kwamba ujumbe wa Mungu ni wa kweli na ni wenye nguvu utaongezeka. Utaimarisha azimio lako la kufuata maadili ya Kikristo hata ukipatwa na jaribu gani. Unaweza pia kuwa mwalimu mwenye matokeo sana. Kwa mfano, unapowafundisha wengine kweli ya Biblia, unaweza kufafanua andiko la 1 Wathesalonike 4:3-7 na kuongeza ufahamu na uthamini wao kwa maadili ya Kikristo. Hivyo, funzo lako linaweza kukusaidia na kuwasaidia wengine wengi wamheshimu Mungu.
-