-
Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Bolivia
Kuhubiri katika eneo la Amazoni huko Bolivia ni kazi ngumu lakini yenye kuridhisha. Kikundi cha ndugu na dada kumi ambao ni mapainia, walijazana kwenye mashua yenye injini. Walibeba mahema, vyombo vya kupikia, na masanduku mengi ya vichapo vya Biblia. Walisafiri umbali wa kilomita 800 hivi kwenye Mto Beni kutoka Rurrenabaque hadi Riberalta. Walitembelea vijiji zaidi ya 70 na kuwaachia watu vitabu zaidi ya 800 na pia broshua na trakti. Waliwaonyesha watu 700 hivi waliopendezwa jinsi ya kujifunza Biblia na wakarudi kujifunza na watu zaidi ya 200 kati yao. Mara nyingi Mashahidi walipokuwa wakiondoka katika vijiji hivyo, watu waliwaambia, “Mnaweza kukaa na kujifunza nasi kwa muda mrefu kidogo?” Katika mji fulani mdogo, mtu mmoja alitaka sana Mashahidi waendelee kujifunza naye na alivunjika moyo walipokuwa wakiondoka. Alisema: “Mmeukata mti. Sasa mnahitaji kuuchonga na kuupiga msasa.”
-
-
Kuhubiri na Kufundisha Duniani Kote2009 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 48]
Ndugu na dada wakifurahia Funzo la “Mnara wa Mlinzi” katika mashua
-