-
Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye TamatiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na wa tatu akamimina bakuli lake ndani ya mito na vibubujiko vya maji. Na hiyo ikawa damu.
-
-
Kasirani ya Mungu Yaletwa Kwenye TamatiUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
7. Ni nini kinachotolewa picha na “mito na vibubujiko vya maji”?
7 Hii “mito na vibubujiko vya maji” ni picha ya yale yaitwayo eti machimbuko ya kisasa hivi ya mwongozo na hekima ambayo hukubaliwa na ulimwengu huu, kama vile falsafa za kisiasa, kiuchumi, kisayansi, kielimu, kijamii, na kidini ambazo huongoza matendo na maamuzi ya binadamu. Badala ya kutegemea Yehova, kwa ajili ya ukweli wenye kutoa uhai, ambaye ndiye Kibubujiko cha uhai, wanadamu ‘wamejichongea wenyewe visima vilivyovunjika’ nao wamekunywa sana “hekima ya ulimwengu huu [ambayo] ni upumbavu kwa Mungu.”—Yeremia 2:13; 1 Wakorintho 1:19; 2:6; 3:19; Zaburi 36:9, NW.
8. Ni katika njia zipi aina ya binadamu imejiletea hatia ya damu?
8 “Maji” kama hayo yaliyochafuliwa yameongoza wanadamu kuwa na hatia ya damu, mathalani, katika kuwatia moyo wamwage damu kwa kadiri kubwa katika vita ambavyo karne iliyopita vilitwaa maisha zaidi ya milioni mia moja. Hususa katika Jumuiya ya Wakristo, ambako vililipuka vita viwili vya ulimwengu, wanadamu wamekuwa “katika uharaka wa kumwaga damu isiyo na hatia,” na hiyo imetia ndani damu ya mashahidi wa Mungu mwenyewe. (Isaya 59:7; Yeremia 2:34, NW) Aina ya binadamu imejiletea pia hatia ya damu kwa kutumia vibaya kiasi kikubwa mno cha damu kwa ajili ya kutia mishipani, katika kukiuka sheria za Yehova za uadilifu. (Mwanzo 9:3-5; Walawi 17:14; Matendo 15:28, 29) Kwa sababu hiyo, kupitia kutiwa damu mishipani, tayari wao wamevuna sikitiko la kuwa na UKIMWI, ugonjwa wa kufura ini, na magonjwa mengine. Lipo kamili kwa ajili ya hatia ya damu litakuja karibuni wakati wakiukaji watakapolipa adhabu iliyo kuu zaidi, wakikanyagwa katika “shinikizo la divai ya kasirani ya Mungu.”—Ufunuo 14:19, 20, NW.
9. Kumiminwa kwa bakuli la tatu kunahusu nini?
9 Katika siku ya Musa, wakati Mto Naili ulipogeuzwa kuwa damu, Wamisri waliweza kuendelea kuwa hai kwa kutafuta machimbuko mengine ya maji. (Kutoka 7:24) Ingawa hivyo, leo, katika pindi ya tauni hii ya kiroho, hakuna mahali katika ulimwengu wa Shetani ambako watu wanaweza kupata maji yenye kutoa uhai. ‘Kumiminwa’ kwa bakuli hili la tatu kunahusu kupiga mbiu kwamba “mito na vibubujiko vya maji” vya ulimwengu viko kama damu, vikileta kifo cha kiroho kwa wote wanaoyanywa. Watu wasipomwendea Yehova, wanavuna hukumu yake mbaya.—Linga Ezekieli 33:11.
-