Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Paradiso ya Kiroho Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Machi 1
    • Alipokuwa na umri wa miaka 12, Gustavo aliamua kwamba alitaka kuwa kasisi wa Katoliki ya Kiroma. Kwa kibali cha wazazi wake, aliingia katika seminari ya kidini. Alipokuwa huko alijiingiza katika muziki, michezo ya kuigiza, na siasa, ambazo zilikuwa zikiendelezwa na kanisa ili kuwavutia vijana. Alijua kwamba kasisi alipaswa kujitoa kwa ajili ya watu na kwamba hangeoa. Lakini, baadhi ya makasisi na wanaseminari ambao Gustavo alijua walijiingiza katika mazoea ya ukosefu wa adili. Katika hali hizo, Gustavo akaanza kulewa kupindukia. Ni wazi, hakuwa amepata paradiso ya kiroho.

      Siku moja, Gustavo alisoma trakti ya Biblia iliyoongea kuhusu paradiso ya kidunia. Ilimfanya afikiri kuhusu kusudi la maisha. Yeye anasema: “Nilianza kusoma Biblia kwa ukawaida, lakini sikuielewa. Hata sikuona kwamba Mungu ana jina.” Aliacha seminari na akawaendea Mashahidi wa Yehova, akitafuta msaada wakuelewa Biblia. Baada ya hapo, alifanya maendeleo haraka na upesi akaweka maisha yake wakfu kwa Mungu. Gustavo alikuwa anajifunza juu ya paradiso ya kiroho.

  • Paradiso ya Kiroho Ni Nini?
    Mnara wa Mlinzi—2001 | Machi 1
    • Hata hivyo, kwa nini Gustavo alihisi kwamba amepata paradiso ya kiroho aliposhirikiana na Mashahidi wa Yehova? Anasema hivi: “Nililinganisha yale niliyoona ulimwenguni na hasa katika seminari na yale niliyopata miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Tofauti kubwa zaidi ni upendo miongoni mwa Mashahidi.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki