Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mambo Makuu Katika Barua kwa Waroma
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Juni 15
    • WANATANGAZWA KUWA WAADILIFU—JINSI GANI?

      (Rom. 1:1–11:36)

      Paulo anaandika hivi: “Wote wamefanya dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu, nayo ni zawadi ya bure kwamba wanatangazwa [na Mungu] kuwa waadilifu kwa fadhili zake zisizostahiliwa kupitia kuachiliwa huru kwa njia ya fidia ambayo Kristo Yesu alilipa.” Pia, Paulo anasema hivi: “Mtu hutangazwa kuwa mwadilifu kwa imani bila matendo ya sheria.” (Rom. 3:23, 24, 28) Kupitia imani katika “tendo moja la kutetewa kuwa haki,” Wakristo watiwa-mafuta na washiriki wa “umati mkubwa” wa “kondoo wengine” wanaweza ‘kutangazwa kuwa waadilifu,’ yaani, watiwa-mafuta kwa ajili ya uzima wa mbinguni wakiwa warithi pamoja na Kristo huku washiriki wa umati mkubwa wakiwa marafiki wa Mungu, wakitarajia kuokoka “ile dhiki kuu.”—Rom. 5:18; Ufu. 7:9, 14; Yoh. 10:16; Yak. 2:21-24; Mt. 25:46.

      Paulo anauliza hivi: “Je, tufanye dhambi kwa sababu hatuko chini ya sheria bali chini ya fadhili zisizostahiliwa?” Anajibu hivi: “Hilo lisitendeke kamwe!” Paulo anaeleza hivi: “Ninyi ni watumwa . . . , ama watumwa wa dhambi kwa kutazamia kifo ama wa utii kwa kutazamia uadilifu.” (Rom. 6:15, 16) “Mkiyaua mazoea ya mwili kwa roho, mtaishi,” anasema.—Rom. 8:13.

  • Mambo Makuu Katika Barua kwa Waroma
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Juni 15
    • KUONYESHA MAISHANI KWAMBA TUMETANGAZWA KUWA WAADILIFU

      (Rom. 12:1–16:27)

      Paulo anasema hivi: “Kwa sababu hiyo nawasihi ninyi kwa huruma za Mungu, akina ndugu, mtoe miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu.” (Rom. 12:1) “Kwa sababu hiyo,” au kwa kuwa Wakristo wanatangazwa kuwa waadilifu kwa sababu ya imani yao, yale ambayo Paulo anasema sasa yanapaswa kubadili mtazamo wao kujielekea, kuelekea wengine, na kuelekea mamlaka za serikali.

      Paulo anaandika hivi: “Namwambia kila mtu hapo kati yenu asijifikirie mwenyewe zaidi kuliko ilivyo lazima kufikiri.” Kisha anatoa himizo hili: “Upendo wenu na uwe bila unafiki.” (Rom. 12:3, 9) “Kila nafsi na ijitiishe kwa mamlaka zilizo kubwa.” (Rom. 13:1) Kuhusu mambo ya dhamiri, Paulo anawatia moyo Wakristo ‘wasiwe wakihukumiana.’—Rom. 14:13.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki