-
Kuishi Kulingana na Sheria ya KristoMnara wa Mlinzi—1996 | Septemba 1
-
-
Tengenezo la Yehova, na pia makutaniko moja-moja, lazima liweke kanuni na taratibu za lazima ili kudumisha utaratibu mzuri. (1 Wakorintho 14:33, 40) Kwani, Wakristo hata hawangekutana pamoja ikiwa hawakuwa na kanuni zozote juu ya wakati, mahali, na jinsi ya kufanya mikutano hiyo! (Waebrania 10:24, 25) Kushirikiana na miongozo yenye kiasi iliyotolewa na wale waliopewa mamlaka katika tengenezo ni sehemu pia ya kuitimiza sheria ya Kristo.—Waebrania 13:17.
-
-
Kuishi Kulingana na Sheria ya KristoMnara wa Mlinzi—1996 | Septemba 1
-
-
Katika Kutaniko
8. (a) Mradi wetu kutanikoni uwe nini sikuzote? (b) Ni zipi baadhi ya hali ambazo chini yazo watu fulani wameomba wapewe kanuni au wamejaribu kufanya kanuni?
8 Katika kutaniko ni mradi wetu vilevile kujengana kwa roho ya upendo. (1 Wathesalonike 5:11) Kwa hiyo Wakristo wote wapaswa kuwa waangalifu wasiongezee mizigo ya wengine kwa kujitwalia daraka la kutoa maoni yao wenyewe katika mambo ya uchaguzi wa kibinafsi. Nyakati nyingine, watu fulani huandikia Watch Tower Society wakiomba wapewe kanuni juu ya mambo kama ni maoni gani wapaswayo kuwa nayo juu ya filamu, vitabu, na hata vichezeo hususa. Walakini, Sosaiti haikupewa mamlaka ya kuchunguza mambo hayo na kutoa maamuzi juu yayo. Katika visa vilivyo vingi, hayo ni mambo ambayo kila mtu mmoja-mmoja au kichwa cha familia apaswa kuamua, ikitegemea kupenda kwake kanuni za Biblia. Wengine huelekea kugeuza madokezo na miongozo ya Sosaiti kuwa kanuni. Kwa kielelezo, katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Machi 15, 1996, kulikuwa na makala nzuri iwatiayo moyo wazee kuwafanyia washiriki wa kutaniko ziara za uchungaji za kawaida. Je, kusudi lilikuwa kuweka kanuni? La. Ingawa wale wawezao kufuata madokezo hayo hupata manufaa mengi, wazee fulani hawawezi kufanya hivyo. Vivyo hivyo, ile makala “Maswali Kutoka kwa Wasomaji” katika toleo la Mnara wa Mlinzi la Aprili 1, 1995, ilionya dhidi ya kupunguza adhama ya pindi ya ubatizo kwa kufanya mambo kupita kiasi, kama karamu zisizodhibitiwa au kupanga misherehekeo. Wengine wametumia shauri hilo komavu kupita kiasi, hata wakiweka kanuni kwamba kutuma kadi ya kutia moyo kwenye pindi hiyo kungekuwa kosa!
-