-
Niliingia Kwenye Shindano Bora Zaidi MaishaniAmkeni!—2010 | Septemba
-
-
Nilifurahia kuwaonyesha kwamba Biblia ililinganisha maisha ya Mkristo na shindano la riadha. Tuko kwenye shindano la mbio za kupata zawadi ya uzima wa milele.—2 Timotheo 2:5; 4:7, 8.
Ukweli wa mambo ni kwamba kusudi halisi na furaha maishani inapatikana, si kwa kushinda mashindano ya mbio, bali kwa kufanya mapenzi ya Muumba wetu. Mazungumzo hayo yaliwafanya wanariadha fulani wachunguze tena miradi yao, na baadhi yao wakakubali kweli za Biblia zilizokuwa zimebadili maisha yangu. Kwa furaha, wengi wao wamemtumikia Mungu kwa bidii ileile waliyokuwa nayo walipokuwa wanariadha.
-
-
Niliingia Kwenye Shindano Bora Zaidi MaishaniAmkeni!—2010 | Septemba
-
-
Kwa miaka kadhaa sasa, nimewazoeza watu wengi katika shindano la kupata uzima, “uzima ulio wa kweli” katika ulimwengu mpya wa Mungu. (1 Timotheo 6:19) Ili kuzoeza wanariadha wawe stadi kabisa, unahitaji kuwaelewa vizuri. Lazima mwalimu wao awasaidie kutokeza kabisa sifa zao nzuri na kushinda udhaifu wao. Anahitaji kuwachochea waendelee hadi wafikie uwezo wao kamili.
Nimeshangazwa sana kuona jinsi maisha ya Mkristo yanavyofanana sana na ya mwanariadha, kama mtume Paulo alivyokazia katika barua yake ya kwanza kwa Wakorintho. Mwanariadha mwenye mafanikio anakazia fikira kufanya mazoezi ya kimwili na hawazii tu ushindi. Yeye hujiwekea miradi halisi anayoweza kutimiza na huyafanyia kazi hadi anapoyatimiza. Anapoacha kukazia fikira lengo lake kuu na kuacha kulifanyia kazi, juhudi zake zote huambulia patupu. Vivyo hivyo, Mkristo wa kweli pia anapaswa kukaza fikira.
Pia mwanariadha mwenye mafanikio anahakikisha kwamba anakula chakula kilicho na lishe kwa ukawaida. Hali hiyo ni sawa na ile ya Mkristo wa kweli. Hali mafundisho yasiyo na maadili, chakula kutoka kwenye “meza ya roho waovu,” kama vile mtume Paulo alivyosema. Badala yake, yeye hula chakula bora zaidi cha kiroho kinachoandaliwa na Mungu kupitia Neno lake, Biblia. (1 Wakorintho 10:21) Zaidi ya hilo, matatizo yanapotokea, mwanariadha mwenye mafanikio hudumisha maoni yanayofaa. Yeye hukubali makosa yake na kufanya marekebisho. “Jinsi ninavyokimbia si bila uhakika,” Paulo aliandika. “Lakini naupigapiga mwili wangu,” akasema, ili asikataliwe.—1 Wakorintho 9:24-27.
Mimi pamoja na mke wangu hudumisha afya nzuri ya kimwili kwa kufanya mazoezi kwa ukawaida. Lakini, haturuhusu hilo lituzuie kumtumikia Yehova, aliyewaumba wanadamu kwa njia ya ajabu. (Zaburi 139:14) Pamoja tunakazia macho zawadi ya “uzima ulio wa kweli”—“ule utakaokuja” katika ulimwengu mpya wa Mungu.—1 Timotheo 4:8.
Baada ya kueleza kuhusu ‘wingu la mashahidi’ walioishi kabla ya nyakati za Ukristo, mtume Paulo alihimiza hivi: “Acheni sisi pia tuondoe kila uzito na dhambi ambayo hututatanisha kwa urahisi, na acheni tukimbie kwa uvumilivu shindano la mbio lililowekwa mbele yetu.” (Waebrania 12:1) Hakuna jambo lingine lililo bora zaidi ya hilo, yaani, kukimbia shindano hilo kwa kuwa wote wanaoshiriki watapata baraka za milele.—2 Timotheo 4:7, 8.
-