-
Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Russell Asafiri Ng’ambo
Katika 1891 alizuru Kanada, ambako kupendezwa kwa kutosha kulikuwa kumechochewa tangu 1880 hivi kwamba kusanyiko lililohudhuriwa na 700 lingeweza kufanywa sasa katika Toronto. Pia alisafiri Ulaya katika 1891 ili kuona ni jambo gani lingeweza kufanywa ili kusogeza mbele kuenezwa kwa kweli huko. Safari hiyo ilimpeleka Ireland, Scotland, Uingereza, nyingi za nchi za bara la Ulaya, Urusi (lile eneo liitwalo sasa Moldova), na Mashariki ya Kati.
Alifikia mkataa gani baada ya kuwasiliana na watu katika safari hiyo? “Sisi hatukuona kufunguka au utayari kwa ajili ya kweli katika Urusi . . . Hatukuona jambo lolote la kututia moyo tutumainie vuno lolote katika Italia au Uturuki au Austria au Ujerumani,” akaripoti. “Lakini Norway, Sweden, Denmark, Uswisi, na hasa Uingereza, Ireland, na Scotland, ni mashamba yaliyo tayari na yanangojea kuvunwa. Mashamba hayo yaonekana yakilia, Njooni huku mtusaidie!” Hiyo ilikuwa ile enzi ambayo Kanisa Katoliki lilikuwa lingali likikataza usomaji wa Biblia, wakati Waprotestanti wengi walikuwa wakiacha makanisa yao, na wengi, wakikatishwa tamaa na makanisa, walikuwa wakikataa Biblia kabisa.
Ili kusaidia wale watu waliokuwa na njaa kiroho, baada ya safari ya Ndugu Russell katika 1891, jitihada zilizoongezwa zilifanywa kutafsiri fasihi katika lugha za Ulaya. Pia, mipango ilifanywa ili kuchapa na kuweka akiba ya fasihi katika London ili fasihi hizo ziweze kupatikana kwa urahisi kwa matumizi katika Uingereza. Shamba la Uingereza, lilithibitika kwelikweli kuwa tayari kuvunwa. Kufikia 1900, tayari kulikuwa makutaniko tisa na jumla ya Wanafunzi wa Biblia 138—miongoni mwao makolpota fulani wenye bidii. Wakati Ndugu Russell alipotembelea Uingereza tena katika 1903, watu elfu moja walikusanyika katika Glasgow ili kumsikia akihutubu juu ya “Matumaini na Matarajio ya Mileani,” 800 walihudhuria katika London, na wasikilizaji 500 kufikia 600 katika miji mingine.
Hata hivyo, katika kuthibitisha maoni ya Ndugu Russell, baada ya ziara yake miaka 17 ilipita kabla ya kutaniko la kwanza la Wanafunzi wa Biblia kuundwa katika Italia, katika Pinerolo. Vipi Uturuki? Wakati wa miaka ya mwisho-mwisho ya 1880, Basil Stephanoff alikuwa amehubiri katika Makedonia, katika ile iliyoitwa wakati ule Uturuki ya Ulaya. Ijapokuwa wengine walionekana kuonyesha kupendezwa, wengine kutoka katika wale waliodai kuwa ndugu walitoa ripoti za uwongo, zilizomfanya atiwe gerezani. Haikuwa mpaka 1909 kwamba barua kutoka kwa Mgiriki katika Smirna (sasa Izmir), Uturuki, iliripoti kwamba kikundi huko kilikuwa kikijifunza kwa uthamini vichapo vya Watch Tower. Kwa habari ya Austria, Ndugu Russell mwenyewe alirudi katika 1911 ili kutoa hotuba katika Vienna, ikawa tu kwamba mkutano ulikatizwa na wafanyaghasia. Katika Ujerumani pia, itikio lenye uthamini lilikuja hatua kwa hatua. Lakini Waskandinevia walionyesha kujua zaidi uhitaji wao wa kiroho.
-
-
Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Ramani katika ukurasa wa 407]
(See publication)
Safari za Russell za kwenda kuhubiri Ulaya, kwa kawaida kupitia Uingereza
1891
1903
1908
1909
1910 (mara mbili)
1911 (mara mbili)
1912 (mara mbili)
1913
1914
-