-
Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Safari ya Ulimwengu ili Kuendeleza Kuhubiriwa kwa Habari Njema
Jitihada nyingine kubwa ilifanywa katika 1911-1912 ili kusaidia watu wa nchi za Mashariki. International Bible Students Association lilituma halmashauri ya wanaume saba, ikiongozwa na C. T. Russell, ili wao binafsi wakadirie hali huko. Kokote walikoenda walisema juu ya kusudi la Mungu la kuletea wanadamu baraka kwa njia ya Ufalme wa Kimesiya. Nyakati nyingine wasikilizaji wao walikuwa wachache, lakini katika Filipino na India, kulikuwa maelfu. Wao hawakuunga mkono kampeni iliyopendwa na wengi wakati huo katika Jumuiya ya Wakristo ya kukusanya pesa kwa ajili ya wongofu wa ulimwengu. Waliona kwamba jitihada iliyo nyingi ya wamishonari wa Jumuiya ya Wakristo ilitumiwa katika kuendeleza elimu ya kilimwengu. Lakini Ndugu Russell alisadiki kwamba walichohitaji watu kilikuwa “ile Gospeli ya uandalizi wa upendo wa Mungu wa Ufalme ujao wa Mesiya.” Badala ya kutarajia kuongoa ulimwengu, Wanafunzi wa Biblia walielewa kutoka kwa Maandiko kwamba jambo lililopasa kufanywa wakati huo lilikuwa kutoa ushahidi na kwamba hilo lingetumikia kusudi la kukusanya “wachaguliwa wachache kutoka kwa mataifa yote, jamaa, kabila na lugha ili kushiriki katika jamii ya Bibi-arusi wa [Kristo]—ili kukaa pamoja Naye katika kiti Chake cha ufalme wakati wa miaka elfu, wakishirikiana kuinua jamii nzima ya kibinadamu.”a—Ufu. 5:9, 10; 14:1-5.
Baada ya kutumia wakati katika Japani, China, na Filipino, na kwingineko, hao washiriki wa halmashauri hiyo waliongeza kilometa 6,400 zaidi za safari katika India. Watu fulani mmoja-mmoja waliokuwa wakiishi India walikuwa wamesoma fasihi za Sosaiti nao walikuwa wameandika barua kuonyesha uthamini wao kwa ajili yayo mapema sana kama 1887. Kazi ya kutoa ushahidi kwa bidii ilikuwa imefanywa pia miongoni mwa watu wenye kusema lugha ya Tamil tangu 1905 na kijana mmoja mwanamume ambaye, akiwa mwanafunzi katika Amerika, alikuwa amekutana na Ndugu Russell naye akajifunza kweli. Mwanamume huyo kijana alisaidia kuanzisha vikundi vya funzo la Biblia vipatavyo 40 kusini mwa India. Lakini, baada ya kuhubiria wengine, yeye mwenyewe alipata kupoteza kibali kwa kuacha kufuata viwango vya Kikristo.—Linganisha 1 Wakorintho 9:26, 27.
Hata hivyo, karibu na wakati huohuo, A. J. Joseph, wa Travancore (Kerala), katika kujibiwa ulizo alilokuwa amemuuliza kwa barua Mwadventisti mashuhuri, alipelekewa buku la Studies in the Scriptures. Humo alipata majibu ya Kimaandiko yenye kuridhisha kwa maswali yake juu ya Utatu. Upesi yeye na washiriki wa familia yake walitoka kwenda kwenye mashamba ya mpunga na minazi ya kusini mwa India wakishiriki imani zao mpya walizozipata. Baada ya ziara ya Ndugu Russell katika 1912, Ndugu Joseph alianza utumishi wa wakati wote. Kwa njia ya reli, mkokoteni wenye kukokotwa na ng’ombe, mashua, na kwa miguu, alisafiri kugawanya fasihi za Biblia. Alipokuwa akitoa hotuba za watu wote, mara nyingi zilikatizwa na makasisi na wafuasi wao. Katika Kundara, wakati kasisi “Mkristo” alipokuwa akitumia wafuasi wake kukatiza mkutano kama huo na kumtupia Ndugu Joseph kinyesi, mwanamume muungwana mashuhuri Mhindu alikuja kuona kelele zilikuwa za nini. Alimwuliza kasisi huyo hivi: ‘Je, hicho ndicho kielelezo kilichowekwa na Kristo cha kufuatwa na Wakristo, au je, yale unayofanya ni kama mwenendo wa Mafarisayo wa wakati wa Yesu?’ Kasisi huyo akaondoka.
Kabla ya ile safari ya miezi minne ya ulimwengu ya halmashauri ya IBSA haijakamilishwa, Ndugu Russell alikuwa amepangia R. R. Hollister kuwa mwakilishi wa Sosaiti katika nchi za Mashariki na kuhakikisha kwamba kazi inafanywa ya kueneza kwa vikundi vya watu ujumbe wa uandalizi wa upendo wa Mungu wa Ufalme wa Kimesiya. Trakti za pekee zilitayarishwa katika lugha kumi, na mamilioni yazo yalienezwa kotekote katika India, China, Japani, na Korea na waenezaji wenyeji. Kisha vitabu vilitafsiriwa katika lugha nne kati ya hizo ili kuandaa chakula zaidi cha kiroho kwa wale walioonyesha kupendezwa. Hapa palikuwa na shamba kubwa, na mengi bado yalihitaji kufanywa. Hata hivyo, yale yaliyokuwa yametimizwa kufikia hapo yalikuwa yenye kustaajabisha kwelikweli.
-
-
Sehemu ya 1—Kuwa Mashahidi Hadi Sehemu ya Mbali Zaidi Sana ya DuniaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Picha katika ukurasa wa 420]
C. T. Russell na washirika sita walifunga safari ya ulimwenguni pote katika 1911-1912 ili kuendeleza kazi ya kuhubiri habari njema
-