-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Kufikia katikati ya 1878, Ndugu Russell alikuwa amekuwa, kwa mwaka mmoja na nusu hivi, mhariri-msaidizi wa gazeti Herald of the Morning, ambalo N. H. Barbour alikuwa mhariri mkuu. Lakini wakati Barbour, katika toleo la Agosti 1878 la gazeti lao, alipodharau fundisho la Kimaandiko la fidia, Russell alijibu kwa kutetea kwa juhudi kweli hiyo muhimu ya Biblia.
Chini ya kichwa “Ule Ufuniko,” Barbour alikuwa ametoa kielezi cha jinsi alivyohisi juu ya fundisho hilo, akisema hivi: “Mimi namwambia boi wangu, au mmoja wa watumishi, James aumapo dada yake, wewe kamata inzi, uchome mwili wake kwa sindano umtundike ukutani, nami nitamsamehe James. Hiyo yatolea kielezi fundisho la kutoa kilicho badala.” Ingawa alidai kuamini katika fidia, Barbour alilirejezea kuwa “si la kimaandiko, na lenye kuchukiza sana kwa mawazo yetu yote ya haki”h lile wazo la kwamba kwa kifo chake Kristo alilipa adhabu ya dhambi kwa ajili ya uzao wa Adamu.
Katika toleo lile hasa lililofuata la Herald of the Morning (Septemba 1878), Ndugu Russell alipinga kwa nguvu sana yale ambayo Barbour alikuwa ameandika. Russell alichanganua yale ambayo Maandiko husema kwelikweli na upatani wayo na “ukamilifu wa haki [ya Mungu], na hatimaye rehema na upendo wake mkuu” kama ulivyoonyeshwa kwa njia ya upaji wa fidia. (1 Kor. 15:3; 2 Kor. 5:18, 19; 1 Pet. 2:24; 3:18; 1 Yoh. 2:2) Kufikia masika yaliyofuata, baada ya jitihada nyingi za kusaidia Barbour aone mambo Kimaandiko, Russell aliacha kutegemeza Herald kifedha; na kuanzia toleo la Juni 1879, jina lake halikuonekana tena akiwa mhariri-msaidizi wa kichapo hicho.
-
-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
h Barbour alidai kuamini katika fidia, kwamba Kristo alikufa kwa ajili yetu. Alilokataa ni wazo la “kutoa kilicho badala”—kwamba Kristo alikufa badala ya sisi, kwamba kwa kifo chake Kristo alilipa adhabu ya dhambi kwa ajili ya uzao wa Adamu.
-