-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Russell alisema hivi juu ya wanaume hao wawili: “Funzo la Neno la Mungu pamoja na ndugu hawa wathaminiwa liliongoza, hatua kwa hatua, ndani ya malisho ya majani mabichi zaidi.” Mmoja, George W. Stetson, alikuwa mwanafunzi mwenye bidii wa Biblia na pasta wa Advent Christian Church katika Edinboro, Pennsylvania.
-
-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
[Sanduku kaitika ukurasa wa 45]
George W. Stetson—“Mtu Mwenye Uwezo Wenye Kutokeza”
C. T. Russell alikubali kwa shukrani usaidizi ambao alipewa na George W. Stetson, wa Edinboro, Pennsylvania, katika kujifunza Maandiko. Stetson alikufa katika Oktoba 9, 1879, akiwa na umri wa miaka 64. Mwezi uliofuata “Watch Tower” lilikuwa na tangazo la kifo cha Stetson ambalo lilifunua staha yenye kina ambayo Russell mwenye umri wa miaka 27 alikuwa nayo kwake. “Ndugu yetu alikuwa mtu mwenye uwezo wenye kutokeza,” akaandika Russell, “na aliacha matarajio maangavu ya heshima za kilimwengu na za kisiasa ili aruhusiwe kuhubiri Kristo.” Ombi la Stetson wakati wa kufa lilikuwa kwamba C. T. Russell atoe mahubiri ya maziko yake; Russell alikubali ombi hilo. “Watu wapatao elfu moja na mia mbili walihudhuria ibada ya maziko,” akaripoti Russell, “hivyo kutoa uthibitisho wa jinsi ndugu yetu alivyokadiriwa kuwa wa maana sana.”—“Watch Tower,” Novemba 1879.
-