Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Betheli ya Brooklyn—Historia ya Miaka 100
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Mei 1
    • Ndugu waliosimamia kazi ya kuhubiri wakati huo walijua kwamba ujumbe wa Biblia uliochapwa katika magazeti ya ulimwengu ulisaidia sana kusambaza kweli za Biblia. Mwaka wa 1908, ujumbe wa Russell kuhusu Biblia ulitokea kila juma katika magazeti 11 ambayo kwa ujumla yalichapisha nakala 402,000.

      Hata hivyo, Russell aliandika: “Ndugu wanaoelewa jinsi makala mbalimbali zinavyosambazwa kati ya magazeti ya ulimwengu . . . wanatuhakikishia kwamba ikiwa yale mahubiri ya kila juma yangeandikwa katika [jiji kubwa] huenda ikawa yangechapishwa kotekote Marekani, na wanakadiria kwamba katika muda wa mwaka mmoja yangekuwa yakichapishwa kwa ukawaida katika mamia ya magazeti.” Kwa hiyo, walianza kutafuta mahali bora kwa ajili ya kupanua kazi ya kuhubiri.

      Kwa nini walichagua Brooklyn? Russell alisema: “Baada ya kusali kuhusu jambo hilo, sote tulikata kauli kwamba eneo la Brooklyn, New York, lenye watu wengi . . . na ambalo linaitwa ‘Mji wa Makanisa,’ linafaa sana kuwa kituo cha kazi ya mavuno.” Matokeo yanaonyesha kwamba uamuzi huo ulikuwa mzuri. Punde si punde, magazeti 2,000 yalikuwa yakichapisha ujumbe wa Biblia wa Russell.

  • Betheli ya Brooklyn—Historia ya Miaka 100
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Mei 1
    • [Picha katika ukurasa wa 22]

      Ujumbe wa Biblia wa Russell uliochapwa katika magazeti

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki