-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Funzo lao la Neno la Mungu liliwasaidia kujua kwamba Muumba ana jina la kibinafsi na kwamba yeye hufanya iwezekane kwa wanadamu kumjua na kufurahia uhusiano wa karibu naye. (1 Nya. 28:9; Isa. 55:6; Yak. 4:8) Watch Tower la Oktoba-Novemba 1881 lilitaja wazi hivi: “YEHOVA ndilo jina litumiwalo si kwa mwingine ila kwa Mtu Mkuu Kupita Wote—Baba yetu, na yeye ambaye Yesu alimwita Baba na Mungu.”—Zab. 83:18; Yn. 20:17.
-
-
Kukua Katika Ujuzi Sahihi Juu ya KweliMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Uthamini Wenye Kukua Kuelekea Jina la Mungu
Hatua kwa hatua hao Wanafunzi wa Biblia walizidi kufahamu umaarufu ambao Maandiko yaliyopuliziwa yalilipa jina la kibinafsi la Mungu. Jina hilo lilikuwa limefichwa katika Kiingereza na tafsiri za Biblia za Douay ya Roma Katoliki na King James ya Protestanti, kama vile baadaye ilivyofanywa na tafsiri kadhaa katika lugha nyingi katika karne ya 20. Lakini tafsiri mbalimbali pamoja na vitabu vya marejezo kwenye Biblia vilishuhudia kwamba jina Yehova lapatikana mara elfu nyingi katika maandishi ya lugha za awali—kwa kweli mara nyingi zaidi ya jina jingine lolote, na mara nyingi zaidi ya jumla iliyounganishwa ya majina ya cheo kama vile Mungu na Bwana. Wakiwa “watu kwa ajili ya jina lake,” uthamini wao wenyewe kuelekea jina hilo la kimungu ulikua. (Mdo. 15:14, NW) Katika The Watch Tower la Januari 1, 1926, walitoa lile walilotambua kuwa suala ambalo lazima kila mtu alikabili, yaani, “Ni Nani Atamheshimu Yehova?”
-