Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Usitawi wa Muundo wa Tengenezo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Kupanga Mambo Kitengenezo ili Habari Njema Zipate Kuhubiriwa

      Katika hatua ya mapema sana, Ndugu Russell alitambua kwamba mojapo madaraka ya maana sana kwa kila mshiriki wa kutaniko la Kikristo lilikuwa kazi ya kueneza evanjeli. (1 Pet. 2:9) Watch Tower lilieleza kwamba maneno ya kiunabii ya Isaya 61:1 hayakuhusu Yesu pekee bali pia wafuasi wake wote watiwa-mafuta kwa roho, yaani: “Bwana amenitia mafuta, niwahubiri wanyenyekevu habari njema,” au, kama vile King James Version hutafsiri nukuu la Yesu la fungu hilo, ‘Amenitia mafuta kuhubiri gospeli.’—Luka 4:18.

      Mapema sana kama 1881, Watch Tower lilikuwa na makala “Wahubiri 1,000 Watakwa.” Hiyo ilikuwa sihi kwa kila mshiriki wa kutaniko atumie wakati wowote ambao angeweza (nusu saa, saa moja, au mbili, au tatu) kushiriki katika kueneza kweli ya Biblia. Wanaume na wanawake ambao hawakuwa na familia zilizowategemea na ambao wangeweza kutoa kabisa nusu au zaidi ya wakati wao kwa kazi ya Bwana walitiwa moyo waanze kazi wakiwa waeneza-evanjeli makolpota. Idadi hiyo ilitofautiana sana mwaka mmoja na mwingine, lakini kufikia 1885 kulikuwa tayari kama 300 waliokuwa wakishiriki kazi hiyo wakiwa makolpota. Baadhi yao pia walishiriki lakini kwa kadiri ndogo zaidi. Madokezo yalitolewa kwa makolpota kuhusu jinsi ya kufanya kazi yao. Lakini shamba lilikuwa kubwa, na angalau mwanzoni, waliteua eneo lao wenyewe na kwenda toka eneo moja hadi jingine sanasana kama walivyoona kuwa vema. Halafu walipokutana kwenye mikusanyiko, walikuwa wakifanya marekebisho yaliyohitajiwa ili kuratibu jitihada zao.

      Mwaka huohuo ambao utumishi wa kolpota ulianza, Ndugu Russell alichapisha idadi fulani ya trakti (au vijitabu) vigawanywe bila malipo. Chenye kutokeza miongoni mwazo kilikuwa kile kijitabu Food for Thinking Christians, kilichogawanywa kufikia idadi ya nakala 1,200,000 katika miezi minne ya kwanza. Kazi iliyohusika katika kupanga uchapaji na ugawanyaji huo ndiyo iliyosababisha kufanyizwa kwa Zion’s Watch Tower Tract Society ili kuangalia mambo ya muhimu. Kuzuia kukatizwa kwa kazi ikiwa kifo chake chatukia, na ili kurahisisha kushughulikiwa kwa michango ipaswayo kutumiwa katika kazi, Ndugu Russell aliomba Sosaiti isajiliwe kisheria, na jambo hilo lilitiwa katika rekodi Desemba 15, 1884. Jambo hilo lilitokeza chombo cha kisheria kilichohitajiwa.

      Uhitaji ulipozuka, ofisi za tawi za Watch Tower Society zilianzishwa katika nchi nyinginezo. Ya kwanza ilikuwa katika London, Uingereza, katika Aprili 23, 1900. Nyingine, katika Elberfeld, Ujerumani, katika 1902. Miaka miwili baadaye, kwenye ule upande mwingine wa dunia, tawi lilipangwa kitengenezo katika Melbourne, Australia. Wakati wa kuandika kitabu hiki, kuna matawi 99 ulimwenguni pote.

      Ijapokuwa mipango ya kitengenezo iliyohitajiwa ili kutayarisha kiasi kikubwa cha fasihi ya Biblia ilikuwa ikisitawishwa, mwanzoni makutaniko yaliachwa yafanye mipango yao ya kugawanya hadharani habari hiyo. Katika barua yenye tarehe ya Machi 16, 1900, Ndugu Russell alieleza jinsi alivyoliona jambo hilo. Barua hiyo aliyopelekewa “Alexander M. Graham, na Kanisa katika Boston, Mass[achusetts],” ilisema hivi: “Kama vile nyinyi nyote mjuavyo, kusudi langu thabiti ni kuacha kila kampuni ya watu wa Bwana kusimamia mambo yao wenyewe, kulingana na maamuzi yao wenyewe, nikitoa madokezo, si kwa njia ya kuingilia [mambo], bali kwa njia tu ya shauri.” Hilo lilitia ndani si mikutano yao tu bali pia njia ambayo waliendesha huduma yao ya shambani. Hivyo, baada ya kuwapa akina ndugu shauri fulani litumikalo, alimalizia kwa elezo hili: “Hili ni dokezo tu.”

  • Usitawi wa Muundo wa Tengenezo
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Sanduku kaitika ukurasa wa 211]

      Ni Kazi ya Nani?

      Kuelekea mwisho wa maisha yake ya kidunia, Charles Taze Russell aliandika hivi: “Ni mara nyingi mno watu wa Mungu husahau kwamba Bwana Mwenyewe ndiye anayeongoza kazi Yake. Mara nyingi mno wazo ni, Sisi tutafanya kazi na kumfanya Mungu ashirikiane nasi katika kazi yetu. Acheni tupate maoni sahihi juu ya jambo hili, na kutambua kwamba Mungu amekusudia na anatimiza kazi kubwa; na kwamba itafanikiwa, kabisakabisa bila kujali sisi na jitihada zetu; na kwamba ni pendeleo kubwa walilopewa watu wa Mungu kushirikiana kufanya kazi na Mfanyi wao katika kutimiza mipango Yake, makusudio Yake, Aliyoratibu, kwa njia Yake. Kwa kuyatazama mambo kwa maoni hayo, sala zetu na kukesha kwetu kwapaswa kuwe kwa kusudi la kujua na kufanya mapenzi ya Bwana, tukiridhika na daraka lolote tupewalo, kwa kuwa ni Mungu wetu atuongozaye. Hii ndiyo programu ambayo Watch Tower Bible and Tract Society imejaribu kufuata.”—“The Watch Tower,” Mei 1, 1915.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki