-
“Wao Si Sehemu ya Ulimwengu”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Wakati huo walielewa kwamba “mamlaka za juu zaidi,” zirejezewazo kwenye Warumi 13:1-7 (KJ), ilikuwa ni watawala wa kilimwengu. Kupatana na hilo, walihimiza kustahi wakuu wa serikali. Katika kuzungumzia Warumi 13:7, C. T. Russell, katika kitabu The New Creation (kilichotangazwa katika 1904), alitaarifu kwamba Wakristo wa kweli “wangekuwa kiasili ndio wenye moyo mweupe zaidi katika kutambua wakuu wa ulimwengu huu, na wenye kutii zaidi sheria na matakwa ya sheria, isipokuwa mahali ambapo hizo zingepatikana zikihitilafiana na matakwa na amri za kimbingu. Ni watawala wachache wa kidunia ikiwa wako ambao watalaumu utambuzi wa Muumba mkuu zaidi na utii mkuu zaidi kwa amri zake. Kwa hiyo, [Wakristo wa kweli] wapaswa kupatikana miongoni mwa wale wenye kutii sheria zaidi wa wakati huu—si wachochezi, si wagomvi, si walaumuo.”
-
-
“Wao Si Sehemu ya Ulimwengu”Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Ijapokuwa walijaribu kufanya lile ambalo walihisi kuwa lenye kumpendeza Mungu, sikuzote msimamo wao haukuwa wa kutokuwamo kabisa. Yale waliyofanya yaliongozwa na imani, waliyoshiriki pamoja na wengine waliodai kuwa Wakristo, kwamba “mamlaka za juu zaidi” zilikuwa “zimeagizwa rasmi na Mungu,” kulingana na maneno ya King James Version. (Rum. 13:1) Hivyo, kupatana na mbiu iliyopigwa na rais wa Marekani, The Watch Tower lilihimiza Wanafunzi wa Biblia wajiunge katika kushika Mei 30, 1918, kuwa siku ya sala na dua kuhusiana na matokeo ya vita ya ulimwengu.a
-