-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
“Inaonekana ni kwa tukio lisilotazamiwa tu kwamba, jioni moja niliingia ndani ya jumba lililochakaa, lenye vumbi, mahali nilipokuwa nimesikia kwamba ibada za kidini zilikuwa zikiendeshwa, ili nione kama watu hao wachache waliokutana humo walikuwa na jambo la akili la kutoa kuliko zile itikadi za kidini za yale makanisa makuu. Humo, kwa mara ya kwanza, nikasikia jambo fulani juu ya maoni ya Waadventisti wa Pili [Advent Christian Church], mhubiri akiwa ni Bw. Jonas Wendell . . . Hivyo, nakiri kuwa na deni kwa Waadventisti pamoja na madhehebu nyinginezo. Ingawa maelezo yake ya Maandiko hayakuwa wazi kabisa, . . . yalitosha, chini ya Mungu, kuimarisha tena imani yangu yenye kuyumbayumba katika kupuliziwa kimungu kwa Biblia, na kuonyesha kwamba maandishi ya mitume na ya manabii yameunganika yasiweze kutenganika. Niliyosikia yaliniingiza katika Biblia yangu nijifunze kwa bidii na uangalifu zaidi kuliko nilivyopata kufanya, nami nitamshukuru Bwana sikuzote kwa ajili ya mwongozo huo; kwa kuwa ingawa Uadventisti haukuniongoza kwenye kweli yoyote moja, ulinisaidia sana katika kuondolea mbali makosa, na hivyo kunitayarisha kwa ajili ya ile Kweli.”
-
-
Kupiga Mbiu ya Kurudi kwa BwanaMashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
-
-
Russell aliandika: “Tulihisi tumehuzunishwa sana na kosa la Waadventisti wa Pili, ambao walikuwa wakimtarajia Kristo katika mwili, na kufundisha kwamba ulimwengu na vyote vilivyomo isipokuwa Waadventisti wa Pili ungeteketezwa.”
-