-
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya BwanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
4. (a) Ni tangu lini watu wa Yehova walikuwa wamekuwa wakitaraji kwamba matukio yenye kuleta uharibifu yangeanza katika 1914? (b) 1914 ungetia alama ya mwisho wa kipindi gani cha wakati?
4 Kuanzia miaka ya katikati ya 1870 watu wa Yehova walikuwa wamekuwa wakitaraji kwamba matukio yenye kuleta uharibifu yangeanza katika 1914 nayo yangeonyesha mwisho wa Majira ya Mataifa. Hiki ndicho kipindi cha “nyakati saba” (miaka 2,520) kikianza na kupinduliwa kwa ufalme wa Kidaudi katika Yerusalemu katika 607 K.W.K. hadi kuketishwa kwa Yesu juu ya kiti cha ufalme katika Yerusalemu la kimbingu katika 1914 W.K.—Danieli 4:24, 25; Luka 21:24.b
5. (a) Ni tangazo gani alilofanya C. T. Russell katika Oktoba 2, 1914? (b) Ni mabadiliko makubwa gani ya kisiasa ambayo yametukia tangu 1914?
5 Hivyo, wakati C. T. Russell alipoonekana kwa ajili ya ibada ya asubuhi pamoja na jamaa ya Betheli ya Brooklyn, New York, asubuhi ya Oktoba 2, 1914, yeye alifanya tangazo hili lenye kusisimua: “Majira ya Mataifa yamekwisha; siku ya wafalme wayo imekwisha.”
-
-
Matetemeko ya Dunia Katika Siku ya BwanaUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Ilikuwa katika K.K. 606, kwamba ufalme wa Mungu ulikwisha, taji liliondolewa, na dunia yote ikapewa Wasio Wayahudi. Miaka 2520 kutoka K.K. 606, itakwisha katika M.B. 1914.”f—The Three Worlds, kilichotangazwa 1877, ukurasa 83.
“Ithibati ya Biblia ni wazi na thabiti kwamba ‘Majira ya Mataifa’ ni kipindi cha miaka 2520, kutoka K.K. 606 kufika na kutia ndani M.B. 1914”—Studies in the Scriptures, Buku 2, kilichoandikwa na C. T. Russell na kikatangazwa 1889, ukurasa 79.
Charles Taze Russell na Wanafunzi wa Biblia wenzake waling’amua miongo kadhaa mapema zaidi kwamba 1914 ungeonyesha mwisho wa Majira ya Mataifa, au nyakati zilizowekwa za mataifa. (Luka 21:24) Ingawa katika siku hizo za mapema wao hawakuelewa kikamili hii ingemaanisha nini, wao walisadikishwa kwamba 1914 ingekuwa tarehe ya mabadiliko katika historia ya ulimwengu, nao walikuwa sahihi.
-