Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Urusi
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • WANATUMIKIA KWA SHANGWE KATIKA MIGAWO YAO

      Arno na Sonja Tüngler ambao walihitimu kutoka Shule ya Gileadi iliyofanyiwa huko Ujerumani, wamekuwa wakitumika katika majiji kadhaa nchini Urusi tangu Oktoba 1993. Kazi ya Yehova imekuwa na matokeo gani katika maeneo ambayo wametumika? Hebu sikiliza masimulizi yao.

      Arno: “Tuliwasili kwenye mgawo wetu huko Moscow. Baada ya majuma machache, tulitoa hotuba zetu za kwanza katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Baada ya kuwa Urusi kwa majuma sita, nilitoa hotuba yangu ya kwanza katika kusanyiko. Tulishirikiana na kutaniko lenye wahubiri waliobatizwa 140 hivi, na eneo la kutaniko hilo lilitoshana na mzunguko mmoja huko Ujerumani! Eneo letu la kwanza lilikuwa karibu na nyumba yetu ya mapainia. Tulifurahi kama nini kuwa Mashahidi wa kwanza kuhubiri eneo hilo nyumba kwa nyumba!”

      Sonja: “Ingawa hatukujua Kirusi, nyakati nyingine tulihubiri barabarani tukiwa peke yetu. Tuliongea na watu na kuwapa trakti na vichapo vingine. Ndugu na dada wa huko walijiunga nasi mara nyingi, na ilikuwa rahisi kupata mtu wa kwenda naye mahubiri. Ndugu hao walituonyesha fadhili na subira na walitusikiliza tulipozungumza Kirusi kisicho sahihi. Wenye nyumba pia walikuwa na subira. Muungano wa Sovieti ulikuwa umeporomoka, na watu walipendezwa sana na dini.”

      Arno: “Kitu kilichotusaidia sana kujifunza Kirusi ni kushiriki katika huduma ya nyumba kwa nyumba na kuongoza mafunzo ya Biblia. Kufikia Januari 1994, mwezi wetu wa nne huko Urusi, tulikuwa tayari tunaongoza mafunzo ya Biblia 22, kwa hiyo tulikuwa na nafasi nyingi za kusikia na kuzungumza Kirusi cha kawaida.

      “Wakati huo, watu wengi sana walibatizwa katika makusanyiko; idadi ya waliobatizwa ingeweza kuwa asilimia 10 au zaidi ya waliohudhuria. Makutaniko kadhaa hayakuwa na ndugu waliostahili kutimiza madaraka ya wazee na watumishi wa huduma. Mzee mmoja alikuwa mwangalizi-msimamizi wa makutaniko matano! Aliniomba nitoe hotuba ya Ukumbusho katika mojawapo ya makutaniko hayo. Watu 804 walihudhuria, na iliwabidi waondoke haraka kwenye jumba hilo kwani kutaniko lingine lilihitaji kutumia jumba hilo. Hata hivyo, msemaji wa kutaniko hilo alipatwa na aksidenti ya barabarani alipokuwa akija kwenye jumba hilo, kwa hiyo hangeweza kufika kwa wakati. Ilinibidi nitoe hotuba ya Ukumbusho tena. Wakati huo, kulikuwa na wahudhuriaji 796! Hivyo, katika makutaniko mawili tu, watu 1,600 walihudhuria Ukumbusho. Hilo linaonyesha jinsi watu wengi walivyopendezwa sana na kweli wakati huo.”

  • Urusi
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • [Picha katika ukurasa wa 224]

      Arno na Sonja Tüngler wamefurahia mapendeleo mengi katika mgawo wao Urusi

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki