-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Ivan Krylov anakumbuka: “Nilipofunguliwa kutoka kambi yenye ulinzi mkali, nilitembelea migodi kadhaa ya makaa ya mawe ambako ndugu na dada zetu walilazimishwa kufanya kazi. Tuliwasiliana na wale waliokuwa wamefaulu kutoa nakala za magazeti yetu na kuwapa wengine nakala hizo. Mashahidi walihubiri katika kila kambi na wengi walipendezwa. Walipoachiliwa wengine walibatizwa katika Mto Vorkuta.”
“Kila mara imani yetu katika Yehova na Ufalme wake ilijaribiwa. Pindi moja mnamo 1948, wafungwa katika kambi moja huko Vorkuta walipanga uasi. Waasi hao waliwaambia wafungwa wengine kwamba wangefaulu kabisa ikiwa wangejipanga katika vikundi, iwe ni vya kitaifa au vya kidini. Kulikuwa na Mashahidi 15 katika kambi hiyo. Tuliwaambia waasi hao kwamba sisi ni Wakristo na hatuwezi kujihusisha katika mambo hayo. Tuliwaeleza kuwa Wakristo wa mapema hawakushiriki katika uasi dhidi ya Waroma. Wengi walishangazwa, lakini tulisimama imara.”
Uasi huo ulitokeza msiba. Askari waliwashinda waasi hao na kuwaingiza katika jengo moja kambini. Kisha wakalimwagilia mafuta na kuliwasha moto. Karibu kila mtu aliyekuwa ndani alikufa. Lakini askari hawakuwaumiza akina ndugu.
Ivan anaendelea kusema: “Mnamo Desemba 1948, nilikutana na ndugu wanane kutoka kambi moja waliokuwa wamefungwa kwa miaka 25. Hali ya hewa ilikuwa mbaya sana katika majira hayo ya baridi kali, nayo kazi kwenye migodi ilikuwa ngumu sana. Hata hivyo, macho ya ndugu hao yalionyesha uhakika na tumaini lenye nguvu. Mtazamo wao uliwaimarisha wafungwa ambao hawakuwa Mashahidi wa Yehova.”
-
-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 100]
Ivan Krylov
-