-
Kuwasaidia Wajane Wakabiliane na Majaribu YaoMnara wa Mlinzi—2001 | Mei 1
-
-
SIMULIZI la Biblia kuhusu Ruthu na mkwe wake Naomi, ni mojawapo ya masimulizi yanayojulikana zaidi kuhusu wajane. Wanawake hao wawili walikuwa wajane. Hata hivyo, mume wa Naomi alikuwa amekufa na vilevile wanawe wawili. Mmoja wa wana hao waliokufa alikuwa mume wa Ruthu. Kwa kuwa waliishi katika jamii iliyotegemea kilimo ambacho kilifanywa hasa na wanaume, hali yao ilikuwa mbaya kwelikweli.—Ruthu 1:1-5, 20, 21.
Hata hivyo, Naomi alikuwa na rafiki wa pekee na mfariji, mkwe wake Ruthu, aliyekataa kumwacha. Baada ya muda, Ruthu akawa ‘anamfaa [Naomi] kuliko wana saba’—si kwa sababu tu ya kumpenda sana Naomi bali pia kwa sababu ya kumpenda Mungu. (Ruthu 4:15) Naomi alipopendekeza Ruthu arudi kwa familia na rafiki zake Wamoabu, Ruthu alijibu kwa maneno ya uaminifu na yenye kugusa moyo zaidi ambayo yamepata kuandikwa: “Wewe uendako nitakwenda, na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu; pale utakapokufa nitakufa nami, na papo hapo nitazikwa; BWANA anitende vivyo na kuzidi, ila kufa tu kutatutenga wewe nami.”—Ruthu 1:16, 17.
Yehova Mungu aliona mtazamo wa Ruthu. Alibariki jamaa ya Naomi na Ruthu iliyokuwa na watu wachache, na hatimaye Ruthu akaolewa na Mwisraeli aliyeitwa Boazi. Mtoto wao, ambaye alikuja kuwa babu ya Yesu Kristo, alitunzwa na Naomi kana kwamba alikuwa wake mwenyewe. Simulizi hilo laonyesha jinsi Yehova anavyowathamini wajane ambao humkaribia na kumtumaini. Zaidi ya hilo, Biblia hutuambia kwamba Yehova huthamini sana wale ambao kwa kuchochewa na upendo husaidia wajane katika majaribu yao. Kwa hiyo, leo twawezaje kutegemeza wajane miongoni mwetu?—Ruthu 4:13, 16-22; Zaburi 68:5.
-
-
Kuwasaidia Wajane Wakabiliane na Majaribu YaoMnara wa Mlinzi—2001 | Mei 1
-
-
Ingawa Ruthu alikuwa mjane kwa kipindi fulani, alimheshimu Naomi kwelikweli kwa hiari na kwa upendo kwa kuhakikisha kwamba amemtimizia Naomi mahitaji yake ya kimwili na ya kihisia-moyo. Kwa kweli, mtazamo wa Ruthu ulimpa sifa njema, hivi kwamba mwanamume aliyekuja kuwa mume wake alimwambia hivi: “Kila mtu katika mji wa watu wangu anakujua ya kwamba u mwanamke mwema.” (Ruthu 3:11, kielezi-chini) Bila shaka, Ruthu alifurahi kumsaidia Naomi kwa sababu Naomi alimpenda Mungu, hakudai mengi mno na alithamini sana jitihada za Ruthu za kumsaidia. Naomi ni kielelezo kizuri kama nini kwa wajane leo!
-