Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tangazeni Mfalme na Ufalme! (1919-1941)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Karibu katikati ya Desemba, Nathan H. Knorr, Frederick W. Franz, na Hayden C. Covington waliwasili kutoka Brooklyn. Hazel Burford, aliyemtunza Ndugu Rutherford wakati wa siku hizo zenye huzuni na zenye kujaribu, alikumbuka baadaye: “Walitumia siku kadhaa pamoja naye wakipitia ripoti ya mwaka kwa ajili ya Kitabu-Mwaka na mambo mengine ya kitengenezo. Baada ya wao kuondoka, Ndugu Rutherford aliendelea kuwa dhaifu na, kama majuma matatu baadaye, Alhamisi, Januari 8, 1942, alimaliza mwendo wake wa kidunia kwa uaminifu.”i

      Habari ya kifo cha Ndugu Rutherford ilipokewaje katika Betheli? “Mimi sitasahau siku ile tulipopata kujua juu ya kifo cha Ndugu Rutherford,” akakumbuka William A. Elrod, aliyekuwa amekuwa mshiriki wa familia ya Betheli kwa miaka tisa. “Ilikuwa wakati wa adhuhuri familia ilipokusanyika kwa ajili ya chakula cha mchana. Tangazo lilikuwa fupi. Hakukuwa na hotuba zozote. Hakuna mtu aliyepumzika siku hiyo ili kuomboleza. Badala yake, tulirudi kwenye kiwanda na kufanya kazi kwa bidii zaidi kuliko tulivyopata kufanya.”

  • Kujulisha Habari Njema Bila Kuacha (1942-1975)
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • “KWA WAPENDA THEOKRASI WOTE:

      Katika Januari 8, 1942, ndugu yetu mpendwa, J. F. Rutherford, alimaliza mwendo wake wa kidunia kwa uaminifu . . . Ilikuwa shangwe na faraja kwake kuona na kujua kwamba mashahidi wote wa Bwana wanafuata, si binadamu yeyote, bali Mfalme Kristo Yesu akiwa Kiongozi wao, na kwamba watasonga mbele na kazi kwa umoja kamili wa tendo.”—Barua yenye kutangaza kifo cha Ndugu Rutherford.a

      HABARI za kifo cha Ndugu Rutherford zilifika zikiwa mshtuko wa kitambo kwa Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. Wengi walijua kwamba alikuwa amekuwa mgonjwa, lakini hawakutarajia afe upesi hivyo. Walihuzunishwa na kifo cha ndugu yao mpendwa lakini walikuwa wameazimia “kusonga mbele na kazi”—kazi ya kupiga mbiu ya Ufalme wa Mungu. Wao hawakumwona J. F. Rutherford kuwa kiongozi wao. Charles E. Wagner, ambaye alikuwa amefanya kazi katika ofisi ya Ndugu Rutherford, alionelea hivi: “Akina ndugu kila mahali walikuwa wamesitawisha usadikisho imara kwamba kazi ya Yehova haikutegemea binadamu yeyote.” Hata hivyo, mtu fulani alihitajiwa ili abebe madaraka ambayo Ndugu Rutherford alikuwa amebeba akiwa msimamizi wa Watch Tower Society.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki