-
Dhabihu Zilizompendeza MunguMnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 15
-
-
Kulingana na hayo, kitabu kimoja chafafanua “dhabihu” kuwa “sherehe ya kidini ambamo kitu fulani hutolewa kwa mungu fulani ili kuanzisha, kudumisha, au kurudisha uhusiano ufaao kati ya mtu na kile akionacho kuwa kitakatifu.”
-
-
Dhabihu Zilizompendeza MunguMnara wa Mlinzi—2000 | Agosti 15
-
-
9. (a) Abeli aliweka imani katika nini, naye aliionyeshaje? (b) Toleo la Abeli lilitimiza nini?
9 Abeli hakuwa na imani tu kwamba kuna Mungu, imani ambayo huenda Kaini pia alidhihirisha. Abeli alikuwa na imani katika ahadi ya Mungu kuhusu Mbegu fulani ambayo ingewaletea wanadamu waaminifu wokovu. Hakujulishwa jambo hilo lingetimizwaje, lakini ahadi ya Mungu ilimfahamisha Abeli kuwa mtu fulani alipaswa kupondwa kisigino. Naam, yaonekana alifikia mkataa kwamba damu ilipasa kumwagwa—maana hasa ya dhabihu. Abeli alimtolea yule aliye Chanzo cha uhai zawadi iliyohusisha uhai na damu, yaelekea ikiwa wonyesho wa tamaa yake kubwa na matazamio ya kuona kutimizwa kwa ahadi ya Yehova. Wonyesho huo wa imani ndio uliofanya Yehova apendezwe na dhabihu ya Abeli, na kwa kadiri ndogo, ukaonyesha maana halisi ya dhabihu—njia ambayo wanadamu wenye dhambi wanaweza kutumia ili kumkaribia Mungu na kupata kibali chake.—Mwanzo 4:4; Waebrania 11:1, 6.
10. Yehova alidhihirishaje maana ya dhabihu kwa kumwomba Abrahamu amtoe Isaka akiwa dhabihu?
10 Yehova alijulisha wazi, kwa njia yenye kutokeza, maana hasa ya dhabihu alipomwamuru Abrahamu amtoe mwana wake Isaka akiwa toleo la kuchomwa. Ingawa dhabihu hiyo haikutolewa kihalisi, ilifananisha jambo ambalo Yehova angefanya hatimaye—kumtoa Mwana wake mzaliwa-pekee akiwa dhabihu kubwa zaidi iliyopata kutolewa ili kutimiza mapenzi Yake kwa wanadamu. (Yohana 3:16)
-