-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Yehova anasema hivi: “Hatakuwapo tena mtoto wa siku chache, wala mzee asiyetimia siku zake; kwa maana mtoto atakufa mwenye umri wa miaka mia; bali mtenda dhambi mwenye umri wa miaka mia atalaaniwa.” (Isaya 65:20)
-
-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
28. Tunajifunza nini kutokana na maneno ya Yehova juu ya maisha katika ulimwengu mpya chini ya Ufalme wake?
28 Maneno ya Yehova yanatuambia nini juu ya maisha katika ulimwengu mpya unaokuja? Chini ya Ufalme wa Mungu, kila mtoto atakuwa na tarajio la kupata wakati ujao ulio salama. Kifo hakitaua tena mwanamume anayemhofu Mungu akiwa katika umri wake wa ufanisi mkubwa. Bali, wanadamu watiifu watakuwa salama salimini, na wataweza kufurahia maisha. Namna gani watu wowote wanaochagua kumwasi Mungu? Watapoteza pendeleo la uhai. Hata ikiwa mtenda-dhambi anayeasi ana “umri wa miaka mia,” atakufa. Hapo yeye atakuwa “mtoto wa siku chache” akilinganishwa na vile angaliweza kuwa—mtu mwenye maisha yasiyo na kikomo.
-
-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
“Nao watajenga nyumba, na kukaa ndani yake; watapanda mizabibu, na kula matunda yake. Hawatajenga, akakaa mtu mwingine ndani yake; hawatapanda, akala mtu mwingine; maana kama siku za mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wangu, na wateule wangu wataifurahia kazi ya mikono yao muda wa siku nyingi.” (Isaya 65:21, 22)
-
-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Tunaweza kuwa na hakika kwamba amani hiyo itaendelea mpaka ndani ya ile Paradiso halisi. Hata haiwezekani kuwaza kwa usahihi ni maajabu gani ambayo Yehova atafanya katika ulimwengu mpya kwa kuitumia mioyo na mikono ya waabudu wake wenye nia ya kufanya kazi. Itakuwa shangwe iliyoje kujenga nyumba yako mwenyewe kisha kuishi ndani yake! Chini ya utawala wa Ufalme, hakutakuwako upungufu wa kazi ya kuridhisha. Utafurahi kama nini “kujiburudisha kwa mema” ya matunda ya kazi zako mwenyewe sikuzote! (Mhubiri 3:13) Je, tutapata wakati wa kutosha kuifurahia sana kazi ya mikono yetu? Kabisa! Maisha yasiyo na kikomo ya wanadamu waaminifu yatakuwa “kama siku za mti”—maelfu ya miaka, na hata zaidi!
31, 32. (a) Wahamishwa wanaorudi watafurahia baraka zipi? (b) Wanadamu waaminifu watakuwa na tazamio gani katika ulimwengu mpya?
31 Yehova anaeleza juu ya baraka zaidi zinazowangoja wahamishwa wanaorudi: “Hawatajitaabisha kwa kazi bure, wala hawatazaa kwa taabu; kwa sababu wao ni wazao wa hao waliobarikiwa na BWANA, na watoto wao pamoja nao.” (Isaya 65:23) Wayahudi hao waliorudishwa watabarikiwa na Yehova, na kwa hiyo hawatafanya kazi ya bure. Wazazi hawatazaa watoto ili tu wapatwe na kifo cha mapema. Watu wale waliokuwa uhamishoni hawatafurahia baraka za kurudishwa wakiwa peke yao; wazao wao watakuwa pamoja nao. Mungu ana hamu nyingi ya kutimiza mahitaji ya watu wake kiasi cha kuahidi hivi: “Itakuwa ya kwamba, kabla hawajaomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.”—Isaya 65:24.
32 Yehova atatimizaje ahadi hizo katika ulimwengu mpya unaokuja? Tungoje tuone. Yehova hajaeleza jinsi kila kitu kitakavyokuwa, lakini tunaweza kuwa na hakika kwamba wanadamu waaminifu “hawatajitaabisha kwa kazi bure” tena. Umati mkubwa wa waokokaji wa Har-Magedoni na watoto wowote ambao huenda wakawazaa watakuwa na tazamio la maisha marefu ya kuridhisha—uhai wa milele! Hata wale watakaofufuliwa kisha wachague kuishi kupatana na viwango vya Mungu watapata shangwe ya kuwa katika ulimwengu mpya. Yehova atayasikia na kuyatimiza mahitaji yao, hata kuyatazamia. Kwa kweli, Yehova ataufungua mkono wake na kuridhisha “kila kilicho hai matakwa yake.”—Zaburi 145:16.
33. Wayahudi watakapoirudia nchi yao, wanyama wataishije kwa amani?
33 Amani na usalama ambazo zimeahidiwa zitakuwa za kiasi gani? Yehova anamalizia sehemu hii ya unabii kwa kusema hivi: “Mbwa-mwitu na mwana-kondoo watalisha pamoja, na simba atakula majani kama ng’ombe; na mavumbi yatakuwa chakula cha nyoka. Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu mtakatifu wote, asema BWANA.” (Isaya 65:25)
-
-
‘Mkashangilie Daima kwa Ajili ya Hivi Niviumbavyo’Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
Baraka zinazofurahiwa sasa na watu wa Yehova katika paradiso yao ya kiroho zitaendelea mpaka ndani ya Paradiso halisi, ambamo amani itakuwamo miongoni mwa wanadamu, na hali kadhalika miongoni mwa wanyama. Tunaweza kuwa na hakika kwamba lile agizo ambalo Mungu aliwapa wanadamu hapo awali litatimizwa kabisa kwa njia inayofaa, yaani: ‘Kuitiisha nchi; kutawala samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi.’—Mwanzo 1:28.
-