-
2. Dumisha UsafiAmkeni!—2012 | Juni
-
-
● Safisha mboga na matunda.
Huenda vyakula vilichafuliwa na maji machafu, wanyama, kinyesi, au vyakula vingine vibichi kabla ya kuuzwa. Kwa hiyo, hata kama utaondoa maganda ya matunda au mboga, yasafishe kabisa ili kuondoa bakteria hatari. Kufanya hivyo kunachukua muda. Mama mmoja nchini Brazili anayeitwa Daiane anasema hivi, “Ninapotayarisha saladi, huwa siharakishi ili nihakikishe nimeyasafisha majani yote vizuri.”
● Usiweke nyama mbichi pamoja.
Ili kuzuia kuenea kwa bakteria pakia vizuri nyama mbichi ya ng’ombe, kuku, na samaki, na uiweke mbali na vyakula vingine. Tumia ubao tofauti kukatia vyakula hivyo au uoshe ubao huo kwa sabuni na maji moto kabla na baada ya kukatia nyama mbichi au samaki.
-
-
3. Tayarisha na Uhifadhi Chakula VizuriAmkeni!—2012 | Juni
-
-
3. Tayarisha na Uhifadhi Chakula Vizuri
M PISHI mmoja katika Israeli la kale ambaye hakuwa mwangalifu alikusanya maboga ya mwituni ambayo ‘hakuwa anayafahamu.’ Aliyatia ndani ya mchuzi. Walaji, waliohofia kwamba chakula hicho kilikuwa na sumu walilia na kusema: “Kuna kifo ndani ya chungu hiki.”—2 Wafalme 4:38-41.
Kama mfano uliotajwa unavyoonyesha, tunapaswa kuwa waangalifu kuhusu chakula ambacho hakikutayarishwa vizuri kwa kuwa kinaweza kutudhuru au hata kutuua. Kwa hiyo, ili kuzuia magonjwa yanayosababishwa na vyakula, jifunze kutayarisha na kuhifadhi chakula kwa uangalifu. Fikiria mapendekezo manne yafuatayo:
● Nyama iliyoganda isiyeyushwe nje ya friji.
Wizara ya Kilimo ya Marekani inasema kwamba “hata ingawa sehemu ya katikati ya nyama huwa bado imeganda inapoyeyuka nje ya friji, huenda sehemu ya nje ya nyama hiyo ikawa na joto la kati ya nyuzi 4 Selsiasi na nyuzi 60 Selsiasi, kiwango kinachosemwa kuwa hatari kwa sababu bakteria huongezeka haraka.” Badala yake, yeyusha chakula ndani ya friji, kwenye mikrowevu, au kitumbukize ndani ya maji baridi kikiwa kimepakiwa.
● Pika chakula hadi kiive kabisa.
Shirika la Afya Ulimwenguni linasema kwamba “karibu viini vyote hatari hufa chakula kinapopikwa na kuiva kabisa.” Unapopika chakula hakikisha kwamba kinaiva kabisa, hasa ikiwa kina supu au mchuzi.a Kwa kuwa inaweza kuwa vigumu kujua halijoto ya vyakula fulani, wapishi wengi hutumia kifaa cha kupima joto la nyama. Au mtu anaweza kudunga nyama kwa kutumia uma au kuikata katikati ili kuhakikisha kwamba imeiva kabisa.
● Chakula kiliwe punde tu baada ya kupikwa.
Chakula kilichopikwa hakipaswi kuachwa nje kwa muda mrefu, kwa hiyo hakikisha kinaliwa punde tu baada ya kupikwa ili kisiharibike. Chakula baridi kinapaswa kuliwa kikiwa baridi na chakula moto kinapaswa kuliwa kikiwa moto. Ili chakula chako kisipoe, kiweke ndani ya joko lenye halijoto ya nyuzi 93 Selsiasi. Ikiwa huna joko, unaweza kuacha chakula juu ya jiko lisilo na moto mwingi.
-