-
Habari Njema Yazaa Matunda Huko São Tomé na PríncipeMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 15
-
-
Wakati huo hangaiko lao kuu lilikuwa kutafuta uwanja wa kujenga Jumba la Ufalme. Alipopata habari hizo, dada mmoja aitwaye Maria alitoa nusu ya ardhi ambapo nyumba yake ndogo imejengwa. Uwanja huo ulikuwa mkubwa vya kutosha kujenga Jumba kubwa la Ufalme. Maria hakujua kwamba wasitawishaji wa ardhi wenye tamaa walikuwa wakiutaka, kwa kuwa jamaa zake wote walikuwa wamekufa. Siku moja mfanyabiashara fulani mashuhuri alikuja kuzungumza na Maria.
“Mambo ninayosikia kukuhusu si mazuri!” akamwonya. “Ninasikia kwamba umetoa ardhi yako bila malipo. Je, hujui kwamba ardhi hiyo ina thamani kubwa sana kwa kuwa iko katika jiji?”
“Kama ningekubali kukuuzia ardhi hiyo, ungenipa pesa ngapi?” Maria akamwuliza. Mtu huyo alipokosa kujibu, Maria aliendelea kusema: “Hata kama ungenipa pesa zote katika ulimwengu, hazingetosha kwa sababu pesa haziwezi kununua uhai.”
“Huna watoto, sivyo”? mtu huyo akauliza.
Ili kukomesha mazungumzo hayo, Maria alisema: “Ardhi hii ni ya Yehova. Alinikopesha kwa miaka mingi sana nami sasa nimemrudishia. Ninatarajia kuishi milele.” Kisha akamwuliza mtu huyo: “Je, unaweza kutoa uhai wa milele?” Bila kusema lolote mtu huyo aligeuka na kwenda zake.
Matokeo yalikuwa kwamba, jengo zuri la orofa mbili lilijengwa kwa msaada wa ndugu wenye ustadi kutoka Ureno. Jengo hilo lina sehemu iliyo chini ya ardhi, Jumba kubwa la Ufalme, na vyumba vya kuishi. Pia lina madarasa ya kufanyia shule za wazee, watumishi wa huduma, na mapainia. Sasa makutaniko mawili yanafanyia mikutano yao katika jumba hilo, na kulifanya kuwa kituo bora cha kuelimisha watu kwa ajili ya ibada safi katika jiji kuu.
Katika jiji la Mé-Zochi, kulikuwa na kutaniko la wahubiri 60 wenye bidii. Wahubiri hao walihitaji sana Jumba la Ufalme linalofaa kwa sababu mikutano ilifanyiwa katika Jumba la Ufalme la muda lililokuwa katika shamba la ndizi. Baraza la jiji lilijulishwa jambo hilo, na maofisa fulani wenye huruma wakatoa uwanja mzuri kwenye barabara kuu. Jumba zuri la Ufalme lilijengwa kwa muda wa miezi miwili kwa msaada wa ndugu kutoka Ureno, waliotumia ule mpango wa kujenga unaochukua muda mfupi. Wenyeji hawakuamini waliyoona. Mhandisi mmoja kutoka Sweden aliyehusika katika ujenzi fulani jijini alishangaa alipowaona ndugu na dada wakifanya kazi. “Siamini!” akasema. “Mashahidi wa Yehova hapa jijini Mé-Zochi wanatumia mpango wa kujenga unaochukua muda mfupi! Tunapaswa kufanya vivyo hivyo kuhusiana na mjengo wetu.” Watu 232 walihudhuria kuwekwa wakfu kwa Jumba la Ufalme Juni 12, 1999. Jumba hilo linawavutia sana wageni wanaotembelea jiji la Mé-Zochi.
-
-
Habari Njema Yazaa Matunda Huko São Tomé na PríncipeMnara wa Mlinzi—2003 | Oktoba 15
-
-
[Picha katika ukurasa wa 9]
Jumba la Ufalme la kwanza huko São Tomé mwaka wa 1994
[Picha katika ukurasa wa 10]
1. Jumba la Ufalme lililojengwa kwa muda mfupi huko Mé-Zochi
-