Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yule Mwanamke Tasa Ashangilia
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sara anafananisha “mke” wa kimbingu wa Mungu, yaani tengenezo lake la viumbe-roho. Tengenezo hilo la kimbingu linaelezwa kwa kufaa kuwa mke wa Yehova, kwa sababu linashirikiana na Yehova kindani, linanyenyekea ukichwa wake, na linaonyesha ushirikiano kamili katika utimizaji wa makusudi yake. Mke huyo anaitwa pia “Yerusalemu la juu.” (Wagalatia 4:26) “Mwanamke” huyo huyo anatajwa kwenye Mwanzo 3:15, na ameonyeshwa katika njozi kwenye Ufunuo 12:1-6, 13-17.

  • Yule Mwanamke Tasa Ashangilia
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • Sara, yule “mwanamke huru” aliyekuwa mke wa Abrahamu, anafananisha tengenezo la Yehova la viumbe-roho lililo kama mke.

  • Yule Mwanamke Tasa Ashangilia
    Unabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
    • 6. Tengenezo la Mungu la kimbingu lilipitia kipindi kirefu cha utasa katika maana gani?

      6 Tukiwa na habari hizo za msingi, tunaanza kuona maana yenye kina kirefu ya Isaya 54:1. Baada ya miongo ya utasa, Sara alimzaa Isaka akiwa na umri wa miaka 90. Vivyo hivyo, tengenezo la Yehova la kimbingu lilipitia kipindi kirefu cha utasa. Kule nyuma katika Edeni, Yehova aliahidi kwamba “mwanamke” wake angetokeza ile “mbegu.” (Mwanzo 3:15, NW) Miaka zaidi ya 2,000 baadaye, Yehova alifanya agano lake pamoja na Abrahamu kuhusu ile Mbegu ya ahadi. Lakini “mwanamke” wa kimbingu wa Mungu alilazimika kungoja karne nyingi sana kabla ya kutokeza Mbegu hiyo. Hata hivyo, wakati ulifika watoto wa huyo aliyekuwa ‘mwanamke tasa’ wakawa wengi sana kuliko wale wa Israeli wa asili. Mfano unaohusu huyo mwanamke tasa unatusaidia kuona ni kwa nini malaika walikuwa na hamu nyingi sana ya kushuhudia ile Mbegu iliyotabiriwa ikiwasili. (1 Petro 1:12) Hilo lilitukia lini hatimaye?

      7. “Yerusalemu la juu” lilipata pindi ya kushangilia wakati gani, kama vile ilivyotabiriwa kwenye Isaya 54:1, na kwa nini unajibu hivyo?

      7 Kuzaliwa kwa Yesu akiwa mtoto wa kibinadamu hakika kulikuwa pindi ya kushangilia miongoni mwa malaika. (Luka 2:9-14) Lakini hilo silo tukio lililotabiriwa kwenye Isaya 54:1. Yesu alipozaliwa kwa roho takatifu mwaka wa 29 W.K., hapo ndipo alipopata kuwa mwana wa kiroho wa “Yerusalemu la juu,” akikubaliwa na Mungu mwenyewe peupe kuwa yeye ni ‘Mwana wake, mpendwa.’ (Marko 1:10, 11; Waebrania 1:5; 5:4, 5) Hapo ndipo yule “mwanamke” wa kimbingu wa Mungu alipopata sababu ya kushangilia, kwa kutimiza Isaya 54:1. Sasa hatimaye mwanamke huyo akawa ametokeza ile Mbegu iliyoahidiwa, yule Mesiya! Karne zake za utasa zikawa zimekwisha.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki