Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Hatasahau Kazi Yenu Enyi Vijana!
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Aprili 15
    • Fikiria kisa cha Jennifer mwenye umri wa miaka 17. Anasema hivi: “Tulikuwa tukila chakula cha mchana shuleni. Wasichana walioketi karibu nami walikuwa wakizungumza juu ya dini na mmoja wao akaniuliza mimi ni mfuasi wa dini gani.” Je, Jennifer aliogopa alipojibu? Anasema: “Bila shaka niliogopa kwa sababu sikujua watasema nini.” Kwa hiyo Jennifer alifanya nini? Anaendelea: “Niliwaambia wasichana hao kwamba mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Kwanza walishangaa. Yaelekea, walifikiri kwamba Mashahidi wa Yehova si watu wa kawaida. Hilo lilifanya waniulize maswali, nami niliweza kusahihisha maoni fulani yasiyofaa waliyokuwa nayo. Hata baada ya siku hiyo, baadhi ya wasichana walinijia mara kwa mara ili kuuliza maswali.”

      7 Je, Jennifer alighairi kwamba alizungumza kuhusu imani yake? Hata kidogo! Anasema: “Nilifurahi sana baada ya kipindi hicho cha mapumziko ya mchana. Sasa wasichana hao wanaelewa imani ya Mashahidi wa Yehova vizuri zaidi.” Jennifer anatoa ushauri huu: “Ukiona ni vigumu kuwatolea wanafunzi wenzako au walimu ushahidi toa sala fupi. Yehova atakusaidia. Utafurahi kwamba ulitumia vizuri nafasi hiyo kutoa ushahidi.”—1 Petro 3:15.

      8. (a) Sala ilimsaidiaje Nehemia alipokabili hali isiyotazamiwa? (b) Huenda ukahitaji kutoa sala fupi ya moyoni kwa Yehova unapokabili hali zipi shuleni?

      8 Ona kwamba Jennifer anapendekeza ‘utoe sala fupi’ kwa Yehova unapopata nafasi ya kutoa ushahidi kuhusu imani yako. Hivyo ndivyo Nehemia, mnyweshaji wa Mfalme Artashasta wa Uajemi, alivyofanya alipokabili hali isiyotazamiwa. Nehemia alionekana kuwa mwenye huzuni kwa sababu alikuwa ameelezwa juu ya hali mbaya ya Wayahudi na kwamba ukuta na malango ya Yerusalemu yalikuwa yameharibika. Mfalme aliona kwamba Nehemia alikuwa na wasiwasi, basi akamwuliza alikuwa na tatizo gani. Kabla ya kumjibu, Nehemia alisali ili kupata mwongozo. Kisha kwa ujasiri akaomba ruhusa ya kurudi Yerusalemu akasaidie kujenga upya jiji lililobomoka. Artashasta alikubali ombi lake. (Nehemia 2:1-8) Unajifunza nini kutokana na hilo? Ukiwa na wasiwasi unapopata nafasi ya kutoa ushahidi kuhusu imani yako, usikose kutoa sala ya moyoni. Petro aliandika hivi: ‘Mtupieni Yehova hangaiko lenu lote, kwa sababu yeye huwajali nyinyi.’—1 Petro 5:7; Zaburi 55:22.

      “Tayari Kujitetea”

      9. Leah mwenye umri wa miaka 13 aliwezaje kuwaachia wanafunzi wenzake nakala 23 za kitabu Vijana Huuliza?

      9 Fikiria kisa kingine. Leah, mwenye umri wa miaka 13, alikuwa akisoma kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazia wakati wa mapumziko ya mchana shuleni. Anasema: “Wanafunzi wengine walikuwa wakinitazama, punde si punde wanafunzi wengi walisimama nyuma yangu na kutazama. Kisha wakaanza kuuliza maswali kuhusu kitabu hicho.” Wasichana wanne walimwomba Leah kitabu Vijana Huuliza siku hiyo. Muda mfupi baada ya hapo wasichana hao walisoma vitabu hivyo pamoja na wengine, kisha hao pia wakataka nakala zao. Leah aliwaachia wanafunzi wenzake na marafiki wake nakala 23 za kitabu Vijana Huuliza katika majuma machache yaliyofuata. Je, ilikuwa rahisi kwa Leah kutoa ushahidi hapo mwanzoni wengine walipomwuliza juu ya kitabu alichokuwa akisoma? Sivyo! Anasema hivi: “Mwanzoni, nilikuwa na wasiwasi. Hata hivyo, nilisali, na nilijua kwamba Yehova alikuwa pamoja nami.”

      10, 11. Msichana mdogo Mwisraeli aliwezaje kumsaidia mkuu wa jeshi la Siria ajifunze kumhusu Yehova, na mtu huyo alifanya mabadiliko gani baadaye?

      10 Huenda kisa cha Leah kikakukumbusha hali iliyompata msichana mdogo Mwisraeli aliyepelekwa utekwani huko Siria. Mkuu wa jeshi la Siria, Naamani, alikuwa mwenye ukoma. Inawezekana kwamba mke wake ndiye aliyeanzisha mazungumzo yaliyomsukuma huyo msichana mdogo kumweleza imani yake. Alisema: “Laiti bwana wangu angekuwa pamoja na yule nabii aliyeko Samaria! Maana angemponya ukoma wake.”—2 Wafalme 5:1-3.

      11 Kwa sababu ya ujasiri wa msichana huyo mdogo, Naamani alipata kujua kwamba “hakuna Mungu duniani mwote, ila katika Israeli.” Hata aliazimia kwamba ‘hangetoa tena sadaka ya kuteketezwa wala dhabihu kwa miungu mingine, ila kwa BWANA.’ (2 Wafalme 5:15, 17) Bila shaka Yehova alibariki tendo la ujasiri la msichana huyo mdogo. Anaweza, na anataka kuwabariki vijana leo pia. Leah amepata baraka kama hizo. Baada ya muda mfupi, baadhi ya wanafunzi wenzake walimwendea na kumwambia kwamba kitabu Vijana Huuliza kimewasaidia kufanya mabadiliko katika mwenendo wao. Leah anasema, “Nilifurahi kwa sababu nilijua kwamba nilikuwa nikiwasaidia wengine wajifunze kumhusu Yehova na kufanya mabadiliko maishani.”

  • Yehova Hatasahau Kazi Yenu Enyi Vijana!
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Aprili 15
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 20]

      Hata Watoto Wanamsifu Yehova!

      Hata watoto wamefaulu kutoa ushahidi shuleni. Fikiria mambo yafuatayo.

      Wanafunzi wa darasa la tano la Amber mwenye umri wa miaka kumi, walikuwa wakisoma kitabu fulani kuhusu jinsi Wayahudi walivyoshambuliwa na Wanazi wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu. Amber aliamua kumletea mwalimu wake video Purple Triangles. Mwalimu alishangaa kujua kwamba Mashahidi wa Yehova pia waliteswa wakati wa utawala wa Nazi. Mwalimu alionyesha wanafunzi wote video hiyo.

      Alipokuwa na umri wa miaka minane, Alexa aliwaandikia wanafunzi wenzake barua na kuwaeleza kinachofanya asisherehekee Krismasi. Mwalimu wake alivutiwa sana na barua hiyo na akamwomba Alexa aisome mbele ya wanafunzi wenzake na hata wale wa madarasa mengine mawili! Mwishoni mwa barua hiyo alisema: “Mimi nimefundishwa kuwaheshimu watu walio na imani tofauti na yangu, nami nawashukuru kwa kuheshimu msimamo wangu wa kutosherehekea Krismasi.”

      Muda mfupi baada ya kuanza darasa la kwanza, Eric alibeba Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia shuleni na kuomba ruhusa awaonyeshe wanafunzi wenzake. Mwalimu wake alisema: “Mbona usiwasomee wanafunzi hadithi moja?” Eric alifanya hivyo. Baadaye akawaomba wote waliotaka kitabu hicho wainue mikono. Wanafunzi kumi na wanane, pamoja na mwalimu waliinua mikono! Sasa Eric anaona ana eneo lake la pekee la kuhubiri.

      Whitney, aliye na umri wa miaka tisa, anathamini broshua Mashahidi wa Yehova na Elimu.c Anasema: “Mama yangu amekuwa akiwapa walimu wangu broshua hiyo kila mwaka, lakini mwaka huu mimi ndiye niliyewapa. Mwalimu wangu alinichagua kuwa ‘mwanafunzi bora wa juma’ kwa sababu ya kichapo hicho.”

      [Maelezo ya Chini]

      c Vichapo vyote vilivyotajwa vimechapishwa na Mashahidi wa Yehova.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki