Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • Miongoni mwa wale walioalikwa kusaidia kupanga mtaala wa mafunzo alikuwa Albert D. Schroeder, aliyekuwa tayari amepata ujuzi mwingi katika Idara ya Utumishi kwenye makao makuu ya Sosaiti katika Brooklyn na akiwa mwangalizi wa tawi la Sosaiti katika Uingereza. Mtazamo wake unaofaa, vile alivyojitoa mwenyewe kusaidia wengine, na kupendezwa kwa uchangamfu na wanafunzi kuliwafanya wale aliowafunza wampende wakati wa miaka 17 aliyotumikia akiwa msajili na mfunzi katika shule hiyo. Katika 1974 akawa mshiriki wa Baraza Linaloongoza, na mwaka uliofuata alipewa mgawo wa kutumikia katika Halmashauri ya Kufundisha yayo.

      Ndugu Schroeder na wafunzi wenzake (Maxwell Friend, Eduardo Keller, na Victor Blackwell) walipanga mtaala wa mafunzo wa miezi mitano uliokazia funzo la Biblia yenyewe na tengenezo la kitheokrasi, pia mafundisho ya Biblia, kusema mbele ya watu, huduma ya shambani, utumishi wa mishonari, historia ya kidini, sheria ya kimungu, jinsi ya kushughulika na maofisa wa serikali, sheria ya kimataifa, kuweka maandishi, na lugha moja ya kigeni.

  • Wamishonari Wasukuma Mpanuko wa Ulimwenguni Pote
    Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu
    • [Picha katika ukurasa wa 524]

      Albert Schroeder akizungumza na wanafunzi wa Gileadi juu ya sehemu za tabenakulo

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki