Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa Nini Tunaamini Kuna Muumba?
    Amkeni!—2006 | Septemba
    • “Uthibitisho wa Kwamba Chembe Ilibuniwa”

      ◼ PAULA KINCHELOE

      MAELEZO YAKE: Kwa miaka kadhaa nimekuwa nikifanya utafiti wa chembe, biolojia ya molekuli, na mikrobiolojia. Kwa sasa nimeajiriwa na Chuo Kikuu cha Emory, Atlanta, Georgia, Marekani. Pia mimi hujitolea kufundisha Biblia katika eneo fulani la Warusi.

      Kwa miaka minne ya masomo yangu ya biolojia, nilifanya tu utafiti wa chembe na sehemu zake mbalimbali. Kadiri nilivyojifunza kuhusu DNA, RNA, protini, na njia za kuyeyusha chakula, ndivyo nilivyostaajabia utata, utaratibu, na usahihi katika chembe. Na ingawa nilivutiwa na yale ambayo mwanadamu amefaulu kujifunza kuhusu chembe, nilishangazwa hata zaidi kutambua bado kuna mengi sana tusiyoyajua. Ninaamini kuna Mungu kwa sababu kuna uthibitisho kwamba chembe ilibuniwa.

      Kwa kujifunza Biblia nimemfahamu Muumba huyo, yaani, Yehova Mungu. Nasadiki kwamba yeye si Mbuni mwenye akili tu, bali pia Baba mwenye upendo na anayenijali. Biblia inafafanua kusudi la uhai na kutoa taraja la maisha yenye furaha ya wakati ujao.

  • Kwa Nini Tunaamini Kuna Muumba?
    Amkeni!—2006 | Septemba
    • “Sheria Zenye Utaratibu Zilizo Rahisi Sana”

      ◼ ENRIQUE HERNÁNDEZ-LEMUS

      MAELEZO YAKE: Mimi ni mhubiri wa wakati wote wa Mashahidi wa Yehova. Pia mimi ni mtaalamu wa fizikia ya nadharia katika Chuo Kikuu cha Kitaifa cha Mexico. Kwa sasa ninafanya utafiti kuhusu ufafanuzi unaofaa wa jinsi joto linavyohusika katika utendaji wa uvutano wa athari ya joto ambao husababisha kupanuka kwa nyota. Pia nimewahi kuchunguza utata wa mifuatano ya DNA.

      Uhai ni tata sana hivi kwamba haungeweza kujitokeza wenyewe. Kwa mfano, fikiria habari chungu nzima iliyo katika molekuli ya DNA. Uwezekano wa kromosomu moja tu kujitokeza ni mdogo kuliko 1 ikigawanywa mara trilioni 9. Uwezekano huo ni mdogo sana hivi kwamba jambo hilo halingewezekana. Nafikiri ni upuuzi kuamini kwamba nguvu fulani isiyo na utu ingeweza kuumba si kromosomu moja tu, bali pia vitu vyote hai vilivyo tata sana na vyenye kustaajabisha.

      Isitoshe, nichunguzapo utendaji wa vitu, kuanzia vitu vidogo visivyoonekana kwa macho hadi mawingu makubwa angani, ninavutiwa na sheria zenye utaratibu zilizo rahisi sana zinazoviongoza. Uhakika huo unanionyesha kwamba aliyeviumba si Mwanahisabati Stadi tu, bali pia ni Msanii Stadi.

      Mara nyingi watu hushangaa ninapowaambia kwamba mimi ni Shahidi wa Yehova. Nyakati nyingine wao huniuliza ninawezaje kuamini kuna Mungu. Ninaelewa kinachowafanya waulize hivyo, kwani dini nyingi haziwahimizi waumini wao watafute uthibitisho wa mambo wanayofundishwa au wafanye utafiti kuhusu imani zao. Hata hivyo, Biblia inatuhimiza tutumie “uwezo wa kufikiri.” (Methali 3:21) Uhakika kwamba vitu vya asili vimebuniwa kwa akili, kutia ndani uthibitisho unaotolewa na Biblia, umenisadikisha kwamba kuna Mungu anayesikiliza sala zetu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki