-
Kwa Nini Ninafurahia Kufanya WanafunziMnara wa Mlinzi—2007 | Februari 1
-
-
Katika mwaka wa 1957, mimi na Mary Robinson tulipewa mgawo wa kufanya upainia katika eneo lenye viwanda la Rutherglen huko Glasgow, Scotland. Tulihubiri kulipokuwa na ukungu, upepo, mvua, na theluji, lakini jitihada hizo hazikuwa za bure. Siku moja nilikutana na Jessie. Nilifurahi kujifunza naye Biblia. Wally, mume wake, alikuwa Mkomunisti, naye aliniepuka mwanzoni. Wally alipojifunza Biblia na kugundua kwamba ni Ufalme wa Mungu tu ndio utakaowaletea wanadamu hali bora alisisimka. Baada ya muda, wote wawili walianza kazi ya kufanya wanafunzi.
Itikio la Kwanza Linaweza Kudanganya
Baadaye, tulipewa mgawo mpya wa kwenda Paisley, Scotland. Siku moja nilipokuwa nikihubiri huko, mwanamke fulani alifunga mlango kwa kishindo ili nisimhubirie. Lakini baadaye alinitafuta ili kuniomba msamaha. Niliporudi juma lililofuata, alisema hivi: “Nilihisi ni kana kwamba nilikuwa nimemfungia Mungu mlango. Ilinibidi nikutafute.” Mwanamke huyo aliitwa Pearl. Aliniambia kwamba alikuwa amekatishwa tamaa na marafiki na watu wa ukoo hivi kwamba alisali kwa Mungu ili apate rafiki wa kweli. Alisema hivi: “Wakati huo ndipo uliponitembelea. Sasa ninatambua kwamba wewe ndiye rafiki huyo wa kweli.”
Haikuwa rahisi kuwa rafiki ya Pearl. Aliishi juu ya kilima, na nililazimika kupanda kilima hicho kwa miguu. Nilipoenda kumchukua nyumbani kwake ili ahudhurie mkutano wa kwanza, karibu nifagiliwe mbali na upepo na mvua. Nilitupa mwavuli wangu kwa sababu uliraruka-raruka. Miezi sita tu baada ya kunifungia mlango kwa kishindo, Pearl alibatizwa na hivyo kuonyesha kwamba alikuwa amejiweka wakfu kwa Mungu.
Muda mfupi baadaye, mume wake aliamua kujifunza Biblia, na punde si punde, aliandamana nami katika huduma ya nyumba kwa nyumba. Kama kawaida, mvua ilikuwa ikinyesha. Akaniambia, “Usiwe na wasiwasi. Kwa kawaida, ninasimama kwa saa nyingi ili kutazama mpira katika hali ya hewa kama hii, na bila shaka ninaweza kusimama katika mvua kwa ajili ya Yehova.” Sikuzote ninavutiwa na ukakamavu wa Waskoti.
Ni furaha kama nini kurudi huko baada ya makumi ya miaka na kuona kwamba watu wengi kati ya wale niliojifunza nao bado wanavumilia katika imani! Hiyo ndiyo shangwe ya kufanya wanafunzi. (1 Wathesalonike 2:17-20) Katika mwaka wa 1966, baada ya kuwa painia nchini Scotland kwa zaidi ya miaka minane, niliitwa kwenye Shule ya Gileadi (Watchtower Bible School of Gilead) ili kuzoezwa kuwa mmishonari.
-
-
Kwa Nini Ninafurahia Kufanya WanafunziMnara wa Mlinzi—2007 | Februari 1
-
-
[Picha katika ukurasa wa 13]
Kufanya upainia huko Scotland
-