-
“Kifo Kitafanywa Kuwa Si Kitu”Mnara wa Mlinzi—1998 | Julai 1
-
-
15. Yamaanisha nini kusema kwamba wanaofufuliwa “[watahukumiwa] kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika hizo hati-kunjo”?
15 Wenye kufufuliwa “[watahukumiwaje] kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika hizo hati-kunjo kulingana na vitendo vyao”? Hati-kunjo hizo si rekodi ya vitendo vyao vya wakati uliopita; walipokufa, waliondolewa hatia ya dhambi walizofanya maishani mwao. (Waroma 6:7, 23) Hata hivyo, wanadamu wenye kufufuliwa bado watakuwa chini ya dhambi ya Kiadamu. Basi, ni lazima iwe kwamba hati-kunjo hizo zitaeleza kikamili maagizo ya kimungu ambayo wote lazima wafuate ili wanufaike kikamili na dhabihu ya Yesu Kristo.
-
-
“Kifo Kitafanywa Kuwa Si Kitu”Mnara wa Mlinzi—1998 | Julai 1
-
-
13. Ni ono gani la ufufuo linalorekodiwa kwenye Ufunuo 20:12-14?
13 Ono la Yohana juu ya ufufuo wa kidunia limerekodiwa kwenye Ufunuo 20:12-14 hivi: “Nikaona wafu, wakubwa na wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha ufalme, na hati-kunjo zikafunguliwa. Lakini hati-kunjo nyingine ikafunguliwa; hiyo ndiyo hati-kunjo ya uhai. Na hao wafu wakahukumiwa kutokana na mambo yale yaliyoandikwa katika hizo hati-kunjo kulingana na vitendo vyao.
-