-
Yehova Ni “Mfunuaji wa Siri”Mnara wa Mlinzi—2012 | Juni 15
-
-
Yehova Ni “Mfunuaji wa Siri”
“Kwa kweli Mungu wenu ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme na Mfunuaji wa siri.”—DAN. 2:47.
-
-
Yehova Ni “Mfunuaji wa Siri”Mnara wa Mlinzi—2012 | Juni 15
-
-
1, 2. Yehova ametufunulia nini, na kwa nini amefanya hivyo?
NI SERIKALI gani zitakazokuwa zikiitawala dunia wakati Ufalme wa Mungu utakapoukomesha utawala wa wanadamu? Tunajua jibu la swali hilo kwa sababu tumefunuliwa na Yehova Mungu ambaye ni “Mfunuaji wa siri.” Anatuwezesha kutambua serikali hizo kupitia mambo yaliyoandikwa na nabii Danieli na mtume Yohana.
2 Yehova aliwafunulia wanaume hao mfululizo wa maono kuhusu wanyama-mwitu wanaofuatana mmoja baada ya mwingine. Pia alimwambia Danieli maana ya ndoto ya kinabii kuhusu sanamu kubwa sana yenye madini mbalimbali. Yehova alihakikisha kwamba masimulizi hayo yameandikwa na kuhifadhiwa katika Biblia kwa faida yetu. (Rom. 15:4) Alifanya hivyo ili kuimarisha tumaini letu la kwamba hivi karibuni Ufalme wake utazivunja serikali zote za wanadamu.—Dan. 2:44.
-