Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kushikilia kwa Imara Jina la Yesu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 14. (a) Tangu siku za mapema, kundi la Kikristo limelazimika kushindana na akina nani, na mtume Paulo aliwaelezaje? (b) Ni maneno gani ya Yesu yanayopasa kutiiwa na yeyote ambaye huenda ikawa ameelekea kufuata kikundi chenye kujitenga mbali?

      14 Tangu siku za mapema, kundi la Kikristo limekuwa halina budi kushindana na waasi-imani wenye kiburi, ambao kwa usemi laini, wenye kudanganya “husababisha migawanyiko na sababu za kukwaza kinyume cha fundisho” lililoandaliwa kupitia mfereji wa Yehova. (Waroma 16:17, 18, NW) Mtume Paulo alionya juu ya tisho hili karibu katika barua zake zote.a Katika nyakati za ki-siku-hizi, wakati ambapo Yesu amerudishia kundi la Kikristo la kweli usafi na umoja walo, hatari ya farakano inabaki. Kwa sababu hiyo, yeyote ambaye huenda alikuwa ameelekea kufuata kikundi chenye kujitenga mbali, hivyo kufanyiza farakano, apaswa atii maneno yafuatayo ya Yesu: “Kwa hiyo tubu. Usipofanya hivyo, mimi naja kwako upesi, nami nitapiga vita nao kwa upanga mrefu wa kinywa changu.”—Ufunuo 2:16, NW.

  • Kushikilia kwa Imara Jina la Yesu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • 16. (a) Kwa nini wale wanaoyumba-yumba kwa sababu ya uvutano wa waasi-imani inawapasa watubu upesi? (b) Ni nini litakalopata wale wanaokataa kutubu?

      16 Wowote ambao wanayumba-yumba kwa sababu ya uvutano wa waasi-imani wapaswa wawe wepesi kutii mwito wa Yesu wa kutubu! Propaganda ya waasi-imani lazima ikataliwe kuwa ni sumu! Msingi wayo ni husuda na chuki, tofauti na zile kweli zenye uadilifu, safi, na zenye kupendeka ambazo Yesu analisha kundi lake. (Luka 12:42; Wafilipi 1:15, 16; 4:8, 9) Kwa habari ya wale wanaokataa kutubu kweli kweli Bwana Yesu ‘hupiga vita nao kwa upanga mrefu wa kinywa chake.’ Yeye anapepeta watu wake ili kuhifadhi ule umoja ambao kwa ajili yao yeye alisali wakati wa jioni yake ya mwisho pamoja na wanafunzi wake duniani. (Yohana 17:20-23, 26) Kwa kuwa waasi-imani wanakataa lile shauri lenye upendo na msaada unaotolewa na zile nyota zilizo kwenye mkono wake wa kulia, Yesu anawahukumu na kuwaadhibu “kwa ukali ulio mkubwa zaidi sana,” akiwaweka kwenye “giza nje.” Wanatengwa na ushirika, wasitende tena kama chachu miongoni mwa watu wa Mungu.—Mathayo 24:48-51; 25:30; 1 Wakorintho 5:6, 9, 13; Ufunuo 1:16, NW.

  • Kushikilia kwa Imara Jina la Yesu
    Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
    • a Ona pia 1 Wakorintho 3:3, 4, 18, 19; 2 Wakorintho 11:13; Wagalatia 4:9; Waefeso 4:14, 15; Wafilipi 3:18, 19; Wakolosai 2:8; 1 Wathesalonike 3:5; 2 Wathesalonike 2:1-3; 1 Timotheo 6:3-5; 2 Timotheo 2:17; 4:3, 4; Tito 1:13, 14; 3:10; Waebrania 10:26, 27.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki