-
“Hakuwa Akisema Nao Bila Mfano”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
Mahubiri ya Mlimani, yaliyo katika Mathayo 5:3–7:27, ni mfano mzuri unaoonyesha jinsi Yesu alivyotumia mifano mingi. Hesabu moja ilionyesha kwamba kuna mifano zaidi ya 50 katika mahubiri hayo. Kumbuka kwamba mahubiri hayo yanaweza kusomwa kwa sauti kwa dakika 20 hivi. Hivyo, kwa wastani, mfano unatajwa karibu kila sekunde 20!
-
-
“Hakuwa Akisema Nao Bila Mfano”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
Ni kwa njia gani Yesu alitumia ndege na maua kuonyesha kwamba Mungu anatujali?
Kwa mfano, alipowahimiza wanafunzi wake wasihangaikie mahitaji yao ya kila siku, alilinganisha hali yao na “ndege wa mbinguni” na “mayungiyungi ya shamba.” Ndege hawapandi wala kuvuna, na mayungiyungi hayasokoti wala kufuma. Lakini Mungu anawatunza ndege hao na maua. Ni rahisi kuelewa jambo kuu, kwamba, ikiwa Mungu anatunza ndege na maua, bila shaka atawatunza wanadamu ‘wanaoendelea kuutafuta kwanza ufalme.’—Mathayo 6:26, 28-33.
-