-
Maagizo kwa Ndugu Walio na Migawo Katika Mkutano wa UtumishiHuduma ya Ufalme—2010 | Septemba
-
-
◼ Maonyesho na Mahojiano: Maagizo yanaposema onyesha, inamaanisha kwamba ndugu aliye na sehemu hiyo ana daraka la kupanga onyesho; si lazima yeye binafsi ashiriki onyesho. Watu atakaochagua kufanya onyesho wanapaswa kuwa wenye kustahili na walio mfano mzuri. Ikiwezekana, wanapaswa kujulishwa mapema. Haifai kuwatumia wahubiri wapya wasio na uzoefu kuonyesha jinsi kazi ya kuhubiri inavyofanywa eti kwa sababu tu ndugu anataka kuwapa fursa ya kuwa jukwaani, ingawa wengine wao wanaweza kutumiwa kama wenye nyumba. Wahubiri wanaotoa onyesho wasiwaonyeshe wasikilizaji mgongo.
-
-
Maagizo kwa Ndugu Walio na Migawo Katika Mkutano wa UtumishiHuduma ya Ufalme—2010 | Septemba
-
-
Wahubiri walio na maonyesho na watakaohojiwa wanapaswa kufanya mazoezi mapema. Ikiwa ndugu aliye na mgawo anaona kwamba mkutano utapitisha wakati na analazimika kufupisha sehemu yake, ataepuka kuondolea mbali maonyesho na mahojiano. Watumishi wa huduma watashauriana na mratibu wa baraza la wazee kabla ya kuchagua wahubiri atakaowatumia katika maonyesho au mahojiano.
-