-
Utukufu Mkubwa Zaidi wa Nyumba ya YehovaMnara wa Mlinzi—1997 | Januari 1
-
-
13, 14. (a) Ni nini liwezalo kusemwa juu ya ugawanyaji wa vichapo katika mwaka wa 1996? (b) Makutaniko yaweza kufanya mipango gani ya pekee kila mwaka, na unapangaje kushiriki?
13 Ingawa mambo madogo-madogo hayaonekani katika chati ya utumishi, kumekuwa na ongezeko lenye kustahili kuangaliwa katika kugawanywa kwa Biblia, vitabu, na magazeti katika mwaka uliopita. Kwa kielelezo, uangushaji wa magazeti ulimwenguni pote ulionyesha ongezeko la asilimia 19, jumla ya nakala 543,667,923 ziliangushwa. Magazeti yetu hurahisisha mahubiri ya kubadilikana-badilikana—barabarani, katika mabustani, kwenye vituo vya mabasi, katika maeneo ya biashara. Ripoti zaonyesha kwamba katika baadhi ya maeneo yanayohubiriwa Ufalme mara nyingi, watu wa kitaaluma wamevutiwa na ubora wa magazeti yetu na wanakubali mafunzo ya Biblia.
14 Kila mwaka katika mwezi wa Aprili, kwa kawaida makutaniko hupanga utendaji wa magazeti wa pekee, ambao ni kampeni ya siku nzima ya kuhubiri nyumba hadi nyumba na katika sehemu za umma. Je, kutaniko lenu litashiriki katika utendaji huo mwezi wa Aprili 1997? Matoleo ya Aprili yenye kutokeza ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! yametayarishwa, na kutolewa kwayo kwa wakati uleule ulimwenguni pote bila shaka kwatazamiwa kuwe kwenye kuvutia! Katika kisiwa cha Saiprasi, makutaniko, yanapotumia maneno ya shime “fikia kila mtu awezaye kufikiwa kwa ujumbe wa Ufalme,” hata yaliyatimiza kila mwezi kwa kazi ya magazeti iliyoratibiwa hivyo, na kufikia kilele kipya cha 275,359 cha magazeti yaliyoangushwa huo mwaka, ongezeko la asilimia 54.
-
-
Utukufu Mkubwa Zaidi wa Nyumba ya YehovaMnara wa Mlinzi—1997 | Januari 1
-
-
[Chati katika ukurasa wa 18-21]
RIPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WA 1996 YA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNI POTE
(Ona magazeti)
-