-
“Mdogo” Amekuwa “Elfu”Mnara wa Mlinzi—2000 | Januari 1
-
-
Watumishi wa Yehova Wenye Bidii
5. (a) Ni mambo gani yaonyeshayo kwamba bidii ya watu wa Yehova haikupungua? (b) Ni nchi gani zilizokuwa na ongezeko lenye kutokeza mwaka wa 1999? (Ona chati kwenye ukurasa wa 17-20.)
5 Watumishi wa kisasa wa Yehova walionyesha bidii iliyoje kwa muda wote wa karne ya 20! Na licha ya mibano inayoongezeka, bidii yao haikupungua mwaka wa 2000 ulipokuwa ukikaribia. Bado waliichukulia kwa uzito sana amri hii ya Yesu: “[Fanyeni] wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote.” (Mathayo 28:19, 20) Idadi ya wahubiri watendaji wa habari njema katika mwaka wa mwisho wa utumishi katika karne ya 20 ilifikia kilele kipya cha 5,912,492. Walitumia jumla yenye kutokeza ya saa 1,144,566,849 wakiongea na wengine juu ya Mungu na makusudi yake. Walifanya ziara za kurudia 420,047,796 kwa watu wanaopendezwa na wakaongoza mafunzo ya Biblia nyumbani yapatayo 4,433,884 bila malipo. Hiyo ni rekodi nzuri kama nini ya utumishi wenye bidii!
6. Mapainia walifanyiwa mpango gani mpya, kukawa na itikio gani?
6 Mwezi wa Januari mwaka uliopita, Baraza Linaloongoza lilitangaza mabadiliko ya takwa la saa kwa mapainia. Wengi waliitumia nafasi hiyo kuanza utumishi wa painia wa kawaida au msaidizi. Kwa kielelezo, wakati wa miezi minne ya kwanza ya mwaka wa kalenda wa 1999, ofisi ya tawi ya Uholanzi ilipokea maombi ya upainia wa kawaida mara nne zaidi ya kipindi kilekile cha mwaka uliotangulia. Ghana yaripoti hivi: “Tangu takwa jipya la saa za painia lianze kutumika, idadi ya mapainia wetu wa kawaida imezidi kuongezeka.” Katika mwaka wa utumishi wa 1999, idadi ya mapainia ulimwenguni kote ilifikia 738,343—wonyesho wa ajabu wa “bidii kwa kazi zilizo bora.”—Tito 2:14.
7. Yehova amebarikije utendaji wenye bidii wa watumishi wake?
7 Je, Yehova amebariki utendaji huo wenye bidii wa watumishi wake? Ndiyo. Kupitia Isaya yeye asema: “Inua macho yako, utazame pande zote; wote wanakusanyana; wanakujia wewe; wana wako watakuja kutoka mbali. Na binti zako watabebwa nyongani.” (Isaya 60:4) “Wana” na “binti” watiwa-mafuta ambao wamekusanywa bado wanamtumikia Mungu kwa bidii. Na sasa, kondoo wengine wa Yesu wanakusanywa upande wa “wana” na “binti” za Yehova watiwa-mafuta katika nchi na visiwa vya bahari 234.
-
-
“Mdogo” Amekuwa “Elfu”Mnara wa Mlinzi—2000 | Januari 1
-
-
Mwaka uliopita watu 323,439 walibatizwa kwa kuonyesha wakfu wao kwa Yehova, naye bado hajafunga malango.
-