Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Huu Ndio Wakati Muhimu Zaidi wa Kukaa Macho!
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Januari 1
    • Mamilioni Wanafuliza Kulinda

      14. Ni takwimu gani zinazoonyesha kwamba wengi leo wanatii shauri la Petro la kukaa macho?

      14 Je, leo wengi wanatii shauri hilo lililoongozwa na roho ya Mungu la kukaa macho? Ndiyo. Katika mwaka wa utumishi wa 2002, kilele cha wahubiri 6,304,645—ongezeko la asilimia 3.1 kuliko mwaka wa 2001—walithibitisha kwamba walikuwa chonjo kiroho kwa kutumia saa 1,202,381,302 wakizungumza na watu kuhusu Ufalme wa Mungu. Wahubiri hao walifurahia kazi hiyo. Ilikuwa kazi muhimu maishani mwao. Mtazamo wa wengi wao ni kama ule wa Eduardo na Noemi wanaoishi nchini El Salvador.

      15. Ni jambo gani lililoonwa linaloonyesha kwamba wengi wanaendelea kukaa chonjo kiroho nchini El Salvador?

      15 Miaka kadhaa iliyopita, Eduardo na Noemi walizingatia maneno haya ya Paulo: “Mandhari ya ulimwengu huu inabadilika.” (1 Wakorintho 7:31) Walifanya maisha yao kuwa sahili na kuanza kazi ya upainia, yaani, utumishi wa wakati wote. Muda uliposonga walibarikiwa katika njia mbalimbali hata wakawa waangalizi wa mzunguko na wa wilaya. Licha ya kupatwa na matatizo magumu, Eduardo na Noemi wanaamini kwamba walifanya uamuzi unaofaa walipoacha vitu vya kimwili na kuanza huduma ya wakati wote. Wengi wa wahubiri 29,269—kutia ndani mapainia 2,454—nchini El Salvador wameonyesha roho hiyo ya kujidhabihu. Kwa sababu hiyo, nchi hiyo ilikuwa na ongezeko la wahubiri la asilimia 2 mwaka jana.

      16. Ndugu fulani mchanga alionyesha mtazamo gani nchini Côte d’Ivoire?

      16 Nchini Côte d’Ivoire, Mkristo mchanga alionyesha mtazamo kama huo alipoandikia ofisi ya tawi hivi: “Mimi ni mtumishi wa huduma. Lakini siwezi kuwaambia akina ndugu wawe mapainia kwa sababu sijawawekea kielelezo kizuri. Kwa hiyo nimeacha kazi yenye mshahara mzuri na sasa nimejiajiri, na ninapata wakati zaidi wa kuhubiri.” Kijana huyo alikuwa miongoni mwa mapainia 983 wanaotumikia katika nchi ya Côte d’Ivoire, ambayo iliripoti wahubiri 6,701 mwaka jana, ongezeko la asilimia 5.

      17. Shahidi mchanga nchini Ubelgiji alionyeshaje kwamba hakuogopeshwa na ubaguzi?

      17 Hali ya kutovumiliana, upendeleo na ubaguzi unazidi kusababisha matatizo kwa wahubiri wa Ufalme 24,961 nchini Ubelgiji. Hata hivyo, wahubiri hao ni wenye bidii na hawana woga. Wakati Shahidi mwenye umri wa miaka 16 aliposikia Mashahidi wa Yehova wakiitwa madhehebu wakati wa somo la maadili shuleni, aliomba ruhusa ya kueleza maoni ya Mashahidi wa Yehova. Akitumia video Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name na broshua Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Akina Nani?, aliweza kueleza ukweli kuhusu Mashahidi. Wanafunzi walifurahia sana habari hiyo na juma lililofuata wanafunzi wakapewa mtihani ambao walipaswa kujibu maswali kuhusu dini ya Kikristo ya Mashahidi wa Yehova.

      18. Kuna uthibitisho gani kwamba wahubiri nchini Argentina na Msumbiji hawakuacha kumtumikia Yehova kwa sababu ya magumu ya kiuchumi?

      18 Wakristo wengi wanalazimika kukabili matatizo magumu katika siku hizi za mwisho. Hata hivyo, wanajitahidi wasiache utumishi wao. Licha ya magumu ya kiuchumi, Argentina iliripoti kilele kipya cha Mashahidi 126,709 mwaka jana. Bado kuna umaskini mwingi nchini Msumbiji. Hata hivyo, kulikuwa na ongezeko la asilimia 4 na wahubiri 37,563 walishiriki kazi ya kuhubiri. Maisha ni magumu kwa watu wengi nchini Albania, hata hivyo, nchi hiyo iliripoti ongezeko la asilimia 12, na kufikia kilele cha wahubiri 2,708. Ni wazi kwamba roho ya Yehova haizuiwi na hali ngumu wakati watumishi wake wanapotanguliza Ufalme.—Mathayo 6:33.

      19. (a) Ni nini kinachoonyesha kwamba bado kuna watu wenye mfano wa kondoo ambao wanatamani kweli ya Biblia? (b) Ni mambo gani mengine katika ripoti ya kila mwaka yanayoonyesha kwamba watumishi wa Yehova wanaendelea kukaa macho kiroho? (Ona chati kwenye ukurasa wa 12-15.)

      19 Wastani wa mafunzo ya Biblia 5,309,289 ulimwenguni pote yaliyoripotiwa mwaka jana unaonyesha kwamba bado kuna watu wengi wenye mfano wa kondoo wanaotamani kweli ya Biblia. Miongoni mwa kilele kipya cha watu 15,597,746 waliohudhuria Ukumbusho, wengi wao hawamtumikii Yehova. Na waendelee kuzidisha ujuzi na upendo kwa Yehova na kwa ndugu zao. Inafurahisha kuona kwamba “umati mkubwa” wa “kondoo wengine” unaendelea kupata matokeo mazuri huku wakimtumikia Muumba “mchana na usiku katika hekalu lake” pamoja na ndugu zao waliotiwa mafuta kwa roho.—Ufunuo 7:9, 15; Yohana 10:16.

  • Huu Ndio Wakati Muhimu Zaidi wa Kukaa Macho!
    Mnara wa Mlinzi—2003 | Januari 1
    • [Chati katika ukurasa wa 12-15]

      2002 REPOTI YA MWAKA WA UTUMISHI WA MASHAHIDI WA YEHOVA ULIMWENGUNI POTE

      (Ona buku lililojalidiwa)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki