Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kitabu Kinachotegemeka—Sehemu ya 4
    Amkeni!—2011 | Februari
    • Tumaini Linalotegemeka

      Muda mfupi baada ya Muungano wa Umedi na Uajemi kushinda Babiloni, Danieli aliandika unabii ambao unatusaidia kuelewa tukio muhimu sana katika kutimizwa kwa mapenzi ya Mungu kwa wanadamu. Malaika Gabrieli alimwambia Danieli wakati hususa ambao Masihi—ule “uzao” ulioahidiwa kwenye Mwanzo 3:15—angekuja! Malaika wa Mungu alisema: “Tangu kutolewa kwa lile neno la kurudisha na kujenga upya Yerusalemu mpaka Masihi aliye Kiongozi, kutakuwa na majuma 7, pia majuma 62,” jumla ya majuma 69. (Danieli 9:25) Kipindi hicho kilichotabiriwa kilianza wakati gani?

      Ingawa Koreshi aliwaruhusu Wayahudi warudi kwenye nchi yao baada tu ya Babiloni kuanguka, miaka mingi baadaye bado Yerusalemu na kuta zake hazikuwa zimerekebishwa. Katika mwaka wa 455 K.W.K., Mfalme Artashasta alimruhusu Nehemia, mnyweshaji wake Myahudi, arudi Yerusalemu na kuongoza kazi ya kulijenga upya. (Nehemia 2:1-6) Yale majuma 69 yalianza wakati huo.

      Hata hivyo, majuma hayo 69 hayakuwa majuma halisi ya siku saba lakini yalikuwa majuma ya miaka. Kwa kweli, tafsiri fulani za Biblia zinasema “majuma ya miaka” badala ya kusema “majuma.”b (Danieli 9:24, 25) Masihi angekuja baada ya kipindi cha “majuma” 69, kila juma likiwa na urefu wa miaka 7—jumla ya miaka 483. Unabii huo ulitimizwa mwaka wa 29 W.K. Yesu alipobatizwa, miaka 483 ukihesabu kutoka mwaka wa 455 K.W.K.c

  • Kitabu Kinachotegemeka—Sehemu ya 4
    Amkeni!—2011 | Februari
    • b Biblia zifuatazo zinatumia usemi “majuma ya miaka”: Tanakh—A New Translation of the Holy Scriptures, The Complete Bible—An American Translation, na The Bible—Containing the Old and New Testaments, ya James Moffatt.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki