-
Kuisikiliza Dhamiri YakoMnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 15
-
-
Namna gani waseja wawili ambao wanafanya ngono ya kinywa? Matineja wengi wanadai kwamba zoea hilo halina madhara kwa sababu si ngono. Je, Mkristo anaweza kusema kwamba ngono ya kinywa ni zoea safi?
8. Kuhusiana na ngono ya kinywa, Wakristo wanatofautiana jinsi gani na watu wengi ulimwenguni?
8 Andiko la Waebrania 13:4 na la 1 Wakorintho 6:9 linaonyesha kwamba Mungu hakubali uzinzi na uasherati (Kigiriki, por·neiʹa). Uasherati unatia ndani nini? Neno la Kigiriki linatia ndani matumizi ya viungo vya uzazi iwe katika njia ya asili au kwa njia potovu kwa makusudi machafu ya ngono. Neno hilo linatia ndani mahusiano yoyote ya ngono nje ya ndoa inayopatana na Maandiko. Hivyo, por·neiʹa inatia ndani ngono ya kinywa, hata ingawa matineja wengi ulimwenguni wameambiwa au wamekata kauli kwamba ngono ya kinywa inakubalika. Wakristo wa kweli hawaachi maoni na matendo yao yaongozwe na wale “wanaoongea maneno yasiyo na faida, na wanaodanganya akili za watu.” (Tito 1:10) Wanashikamana na viwango vya juu zaidi vya Maandiko Matakatifu. Badala ya kujaribu kutetea ngono ya kinywa, wanaelewa kwamba kulingana na Maandiko ngono ya aina hiyo ni uasherati, por·neiʹa, nao wanazoeza dhamiri yao kukataa zoea hilo.a—Matendo 21:25; 1 Wakorintho 6:18; Waefeso 5:3.
-
-
Kuisikiliza Dhamiri YakoMnara wa Mlinzi—2007 | Oktoba 15
-
-
a Gazeti la Mnara wa Mlinzi la Januari 1, 1984 (1/1/1984), ukurasa wa 7-8, linatoa maelezo kwa ajili ya wale waliofunga ndoa.
-