-
Uhuru wa Kusema Je, Unatumiwa Vibaya?Amkeni!—1996 | Julai 22
-
-
“Mara tu watoto waunganishwapo kwenye mfumo wa kompyuta,” likaonelea gazeti moja la habari la Uingereza, “ponografia zenye ngono halisi hazipatikani tu mahali ambapo itakuwa vigumu kwa watoto kufikia, bali zapatikana kwa utayari kwa mtoto yeyote, na hilo lamaanisha katika usiri wa chumba cha kulala.” Inatabiriwa kwamba asilimia 47 ya nyumba zote za Uingereza zenye kompyuta zitaunganishwa kwa mifumo ya kompyuta kufikia mwisho wa 1996. “Wazazi wengi wa Uingereza hawafahamu vidude vya kitekinolojia kama watoto wao. Katika miezi 18 ambayo imepita ‘kupitia-pitia mfumo wa Internet’ kumekuwa moja ya vipitisha-wakati vya matineja vipendwavyo sana,” gazeti hilo likasema.
Kathleen Mahoney, profesa wa sheria kwenye Chuo Kikuu cha Calgary, Kanada, pamoja na mtaalamu katika masuala ya kisheria yanayohusu ponografia, walisema: “Umma wapaswa kujua kwamba kuna njia isiyodhibitiwa kikamili ambayo kupitia kwayo watoto wanaweza kutendewa vibaya na kutumiwa vibaya.” Ofisa mmoja wa polisi wa Kanada alisema: “Ishara ziko wazi kwamba ongezeko kubwa katika visa vya ponografia ya watoto inayohusiana na kompyuta liko karibu kutukia.” Vikundi vingi vya kushauri familia husisitiza kwamba ponografia ya kompyuta inayoonwa na watoto na uvutano inayoweza kuwa nao juu yao “huwakilisha hatari ya wazi na iliyopo.”
-
-
Uhuru wa Kusema Je, Unatumiwa Vibaya?Amkeni!—1996 | Julai 22
-
-
Profesa mmoja kwenye Shule ya Kisheria ya New York asababu kwamba kuna manufaa katika njia kadhaa za kujieleza kuhusu ngono, nje ya mweneo wa haki za kiraia na uhuru wa kusema. “Ngono kwenye Internet yaweza hasa kuwa nzuri kwa vijana,” Time likaripoti juu ya maoni yake. “[Ulimwengu wa kompyuta] ni mahali salama pa kuvumbua mambo yaliyokatazwa na yaliyo mwiko . . . Huandaa uwezekano wa mazungumzo ya kikweli bila haya kuhusu picha za akilini za kifantasia zilizo sahihi za ngono,” yeye akasema.
-