-
Mashaka Yako Ulimwenguni KoteAmkeni!—1999 | Aprili 8
-
-
Kutendwa vibaya kingono na watu wanaovutiwa kingono na watoto ni tisho jingine linalowakabili watoto ulimwenguni pote. Kijarida Trends & Issues in Crime and Criminal Justice chatoa fasiri hii: “Kuvutiwa kingono na watoto kwarejezea uvutio wa kingono kuelekea mtoto aliye mchanga sana. . . . Sikuzote kuvutiwa kingono na watoto huhusisha kutenda uhalifu kama vile kushambulia kingono, mambo ya aibu na makosa yanayohusisha ponografia ya watoto.”
Ripoti zenye kusikitisha za vikundi vya watu wenye kuvutiwa kingono na watoto, ambao huwatumia watoto vibaya kwa pupa, zinazidi kupokewa kutoka sehemu zote za ulimwengu. (Ona sanduku kwenye ukurasa wa 7.) Wenye kutendwa vibaya ni wavulana na wasichana wachanga. Wakishawishwa na wanaume wasio na adili, wanatendwa vibaya kingono na kisha wanatishwa au kudekezwa kupita kiasi ili kuwachochea wabaki katika “kikundi” hiki. Wanaume ambao hupanga na kufanya matendo haya maovu mara nyingi huwa ni viongozi mashuhuri wa jumuiya na nyakati nyingine hufanya hivyo huku polisi na idara ya mahakama wakiwa na habari za kutosha na kuwalinda.
-
-
Mashaka Yako Ulimwenguni KoteAmkeni!—1999 | Aprili 8
-
-
Utendaji wa Internet Unaofanywa kwa Uangalifu
Miezi michache iliyopita, katika mojawapo ya jitihada kubwa zaidi iliyopata kufanywa ya utendaji wa siri dhidi ya ponografia ya watoto inayopitishwa kwenye Internet, polisi katika nchi 12 walivamia nyumba za washukiwa zaidi ya 100 wenye kuvutiwa kingono na watoto. Kutoka kikundi kimoja tu cha wanaume wenye kuvutiwa kingono na watoto huko Marekani, walitwaa picha za kiponografia za watoto zaidi ya 100,000.
Mpelelezi wa Uingereza aliyeratibu uchunguzi huo wa Internet wa miezi mitano alisema hivi: “Mambo yaliyomo yangemfanya mtu yeyote mwenye akili timamu ashikwe na kichefuchefu.” Kulikuwa na watoto wa jinsia zote mbili, wengine wakiwa na umri wa miaka miwili. Polisi wa Ubelgiji walisema kwamba picha za Internet ndizo zilizokuwa “zenye kunyarafisha zaidi kati ya ponografia ya watoto. . . . Zilikuwa mbaya sana hivi kwamba watu walifikia kiwango cha kuwatenda vibaya watoto wao wenyewe ili waweze kutokeza picha zenye kutazamisha zaidi.” Mtu mmoja alipiga picha zake mwenyewe akimbaka mpwa wake wa kike na kuingiza picha hizi ndani ya kompyuta.
Washukiwa walitia ndani walimu, mwanasayansi, mwanafunzi wa sheria, kiongozi wa maskauti, mhasibu, na profesa wa chuo kikuu.
-