Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Ni Mchungaji Wetu
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 1
    • 6. Kulingana na kamusi moja ya Biblia, mchungaji wa kale alifanya nini siku nzima?

      6 Mchungaji wa kale alifanya nini siku nzima? Kamusi moja ya Biblia inaeleza hivi: “Mapema asubuhi aliwatoa kondoo zizini, kisha akawaongoza hadi malishoni huku akitembea mbele yao. Akiwa huko, aliwachunga siku nzima huku akihakikisha kwamba hakuna kondoo yeyote anayetanga-tanga, na iwapo mmoja wao angeponyoka na kuwaacha wengine bila yeye kujua, angemtafuta kwa bidii mpaka ampate na kumrudisha. . . . Usiku, alirudisha kundi zizini, akiwahesabu huku wakipita mlangoni chini ya fimbo ili kuhakikisha kwamba hakuna aliyekosekana. . . . Mara nyingi alilazimika kulinda zizi usiku ili kondoo wasishambuliwe na wanyama wa mwitu au wezi.”a

      7. Kwa nini wakati mwingine mchungaji alihitaji kuwa mwenye subira na mwenye huruma zaidi?

      7 Wakati mwingine kondoo wenye mimba na wale wachanga walihitaji subira na huruma zaidi. (Mwanzo 33:13) Kitabu kimoja kinachozungumzia Biblia kinasema hivi: “Mara nyingi kondoo huzaliwa mbali sana milimani. Mchungaji humlinda kwa makini mama aliye dhaifu kisha humbeba mwana-kondoo na kumpeleka zizini. Kwa siku kadhaa baada ya kuzaliwa, mpaka atakapoweza kutembea, huenda akambeba mikononi mwake au katika mapindo ya vazi lake la juu.” (Isaya 40:10, 11) Bila shaka, mchungaji mzuri alihitaji kuwa mwenye nguvu na mwenye huruma.

  • Yehova Ni Mchungaji Wetu
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 1
    • a Ona Mwanzo 29:7; Ayubu 30:1; Yeremia 33:13; Luka 15:4; Yohana 10:3, 4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki