-
Mwanavita-Mfalme Asherehekea Ushindi Kwenye Har–MagedoniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
“Na katika kinywa chake unatokeza upanga mkali mrefu kwamba yeye apate kupiga mataifa kwa huo, na yeye atayachunga kwa ufito wa chuma.” (Ufunuo 19:15a, NW)
-
-
Mwanavita-Mfalme Asherehekea Ushindi Kwenye Har–MagedoniUfunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu!
-
-
16. Zaburi na Yeremia huelezaje habari ya daraka la Mwanavita-Mfalme wa Yehova?
16 Mwanavita-Mfalme, akiwa mwekwa rasmi wa Yehova, atafanya utofautisho kati ya wale watakaookoka na wale watakaokufa. Yehova, akisema kiunabii kwa Mwana huyu wa Mungu, anasema: “Wewe utavunja wao [watawala wa dunia] kwa fimbo ya kifalme ya chuma, kana kwamba ni chombo cha mfinyanzi wewe utavunja wao vipande vipande.” Na Yeremia anawaambia viongozi kama hao wafisadi wa kiserikali na watumishi wao, akisema: “Zomeni, nyinyi wachungaji, na kuguta! Na kugaagaa huku na huku, nyinyi wenye fahari ya kifalme wa kundi, kwa sababu siku zenu za kuchinja na za kutawanya kwenu zimetimizwa, na ni lazima nyinyi mwanguke kama chombo chenye kutamanika!” Hata watawala hao wawe wameonekana kuwa wenye kutamanika kama nini kwa ulimwengu mbovu, dharuba moja kutoka kwa fimbo ya kifalme ya Mfalme itawavunjavunja, kama kuvunja chombo chenye kuvutia. Itakuwa kama vile Daudi alitoa unabii kuhusu Bwana Yesu: “Fimbo ya imara yako Yehova atapeleka nje kutoka Sayuni, kusema: ‘Enda hali ukitiisha katikati ya maadui wako.’ Yehova mwenyewe kwenye mkono wako wa kulia kwa hakika atavunja wafalme vipande vipande katika siku ya kasirani yake. Yeye atatekeleza hukumu miongoni mwa mataifa; yeye atasababisha ujazi wa miili mifu.”—Zaburi 2:9, 12; 83:17, 18; 110:1, 2, 5, 6; Yeremia 25:34, NW.
-