Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Kupita Katika Tundu la Sindano’
    Amkeni!—2008 | Novemba
    • Kaburi la Meli

      Kabla ya alfajiri ya Juni 1, 1878 (1/6/1878), meli ya matanga iliyoitwa Loch Ard ilisafiri kwenye ukungu kuelekea pwani ya Victoria. Ukungu huo ulioanza siku iliyotangulia ulimzuia nahodha kujua mahali hususa ambapo meli yake ilikuwa. Kwa sababu hiyo alikuwa karibu na pwani ya Australia kuliko alivyodhani. Kwa ghafula, ukungu uliondoka na akaona miamba yenye urefu wa mita 90 kilomita mbili hivi mbele yake. Mabaharia walijitahidi kuigeuza meli hiyo lakini upepo na mkondo wa bahari ukawazuia. Katika muda wa saa moja hivi, meli hiyo iligonga tumbawe kwa kishindo kikubwa na ikazama dakika 15 baadaye.

      Kati ya watu 54 waliokuwa kwenye meli hiyo, ni wawili tu waliookoka, mfanyakazi wa meli Tom Pearce, na abiria Eva Carmichael. Wote walikuwa na umri usiozidi miaka 20. Kwa muda wa saa nyingi, Tom alishikilia mashua ya kuokoa uhai akiwa ndani ya maji baridi sana. Hatimaye alichukuliwa na mkondo wa maji hadi kwenye korongo lililokuwa katikati ya miamba mikubwa. Alipoona ufuo mdogo uliojaa vipande vya meli, aliogelea hadi ufuoni. Eva hangeweza kuogelea kwa hiyo alishikilia mabaki ya meli kwa saa nne hivi kabla ya kuchukuliwa na mkondo hadi kwenye korongo hilo. Alipomwona Tom ufuoni, alipaaza sauti akiomba msaada. Tom aliruka ndani ya mawimbi makubwa na baada ya kujitahidi kwa saa moja alimburuta Eva aliyekuwa amepoteza fahamu hadi ufuoni. Eva alisimulia hivi: “Alinipeleka ndani ya pango lililokuwa zaidi ya mita 50 kutoka ufuoni na akapata kasha lililokuwa na mvinyo akafungua chupa moja, akaninywesha, na hilo likanifanya nipate fahamu. Alitandika nyasi ndefu na majani fulani ili nilalie. Nilipoteza fahamu kwa saa kadhaa.” Wakati huo, Tom alipanda mwamba huo mkubwa na kwenda kutafuta msaada. Muda usiozidi saa 24 baada ya meli ya Loch Ard kuzama, Tom na Eva walipelekwa katika nyumba iliyokuwa karibu. Wazazi wa Eva, ndugu zake watatu, na dada zake wawili walikufa katika msiba huo.

  • ‘Kupita Katika Tundu la Sindano’
    Amkeni!—2008 | Novemba
    • [Sanduku/Picha katika ukurasa wa 17]

      NI NINI KILICHOWAPATA TOM NA EVA?

      Tom Pearce na Eva Carmichael, waokokaji pekee wa msiba wa meli iliyoitwa Loch Ard, walikuwa maarufu upesi huko Australia. Kitabu Cape Otway—Coast of Secrets kinasema: “Magazeti yalitangaza sana kuhusu msiba huo, Pearce alisifiwa kuwa shujaa, Eva Carmichael akasemwa kuwa mrembo na yakasisitiza kwamba wanapaswa kuoana.” Ingawa Tom aliomba kumwoa, Eva alikataa na kurudi Ireland baada ya miezi mitatu. Akiwa huko aliolewa na kuanzisha familia. Eva alikufa mnamo 1934 akiwa na umri wa miaka 73. Tom alirudi kuabiri baharini na upesi akavunjikiwa na meli kwa mara ya pili. Kwa mara nyingine tena aliokoka. Baada ya kuwa nahodha wa meli zinazoendeshwa kwa mvuke kwa miaka mingi, Tom alikufa mnamo 1909 akiwa na umri wa miaka 50.

      [Hisani]

      Both photos: Flagstaff Hill Maritime Village, Warrnambool

  • ‘Kupita Katika Tundu la Sindano’
    Amkeni!—2008 | Novemba
    • [Picha katika ukurasa wa 16]

      Baada ya kugonga tumbawe, meli inayoitwa “Loch Ard” ilizama baada ya dakika 15

      [Hisani]

      La Trobe Picture Collection, State Library of Victoria

      [Picha katika ukurasa wa 17]

      Mbuga ya Taifa ya Port Cambell mahali ambapo (1) meli inayoitwa “Loch Ard” iligonga tumbawe na (2) pango la Tom Pearce

      [Picha zimeandaliea na]

      Photography Scancolor Australia

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki