Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Urusi
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Mikhail Savitsky anakumbuka hivi: “Mashahidi wa Yehova katika Muungano wa Sovieti walihitaji sana kuwa na umoja wakati huo. Tulimshukuru sana Yehova kwa jinsi alivyotutegemeza kiroho kwa upendo na subira. Mara tu baada ya kusikia makala hiyo ikisomwa, ndugu mmoja aliyekuwa amejitenga na tengenezo aliniambia hivi, ‘Naomba gazeti hilo ili nikalisome pamoja na ndugu wengine huko Bratsk na maeneo mengine.’ Nilimwambia kwamba tulikuwa na gazeti moja tu. Lakini alinihakikishia kwamba atanirudishia baada ya juma moja. Alirudisha gazeti hilo pamoja na ripoti za utumishi za muda mrefu za makutaniko mengi. Mamia ya akina ndugu na dada walirudi katika familia yenye umoja ya waabudu wa Yehova.”

  • Urusi
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Aleksey Gaburyak, aliyekuwa mwangalizi wa mzunguko kuanzia 1986 mpaka 1995, anakumbuka hivi: “Tulikutana na washiriki wa Halmashauri ya Nchi huko Usol’ye-Sibirskoye mwaka wa 1965. Ndugu hao walituomba tuwatafute ndugu na dada wote waliokuwa wametawanyika kwa sababu ya kuhamishwa, kufungwa gerezani, au kwa sababu ya mgawanyiko uliokuwepo na kuwaunganisha tena na makutaniko. Tulipewa anwani kadhaa. Eneo langu lilitia ndani wilaya ya Tomsk na Kemerovo na pia majiji ya Novokuznetsk na Novosibirsk. Ndugu wengine walipewa maeneo tofauti. Tulipaswa kupanga makutaniko na vikundi mbalimbali na pia kuwaweka rasmi na kuwazoeza ndugu wanaostahili. Isitoshe, tulihitaji kupanga jinsi ambavyo vichapo vingewafikia akina ndugu na kupanga mikutano ya kutaniko chini ya marufuku. Kwa muda mfupi tu, tulifanikiwa kuwatembelea ndugu na dada 84 ambao walikuwa wametenganishwa na tengenezo. Jinsi tulivyofurahi kuona kwamba ‘kondoo’ wa Yehova walisikia tena sauti ya Mchungaji Mwema na walimtumikia pamoja na watu wake!”—Yoh. 10:16.

      Muda si muda wengi waliokuwa wametenganishwa na tengenezo walijiunga tena na Halmashauri ya Nchi na wakaanza kutuma ripoti zao za utumishi wa shambani. Kufikia mwaka wa 1971, zaidi ya wahubiri 4,500 walikuwa wamejiunga tena na tengenezo la Yehova. Licha ya marufuku iliyokuwepo, kufikia miaka ya katikati ya 1980, kazi ya kuhubiri ilikuwa ikiendelea na wapya walikuwa wakiongezeka katika makutaniko.

  • Urusi
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Kuchapisha nakala za vichapo vya Biblia haikuwa rahisi, lakini Yehova alibariki kazi hiyo. Kati ya mwaka wa 1949 na 1950, akina ndugu walichapisha na kusambaza nakala 47,165 za vichapo mbalimbali kwenye makutaniko. Kuongezea hilo, licha ya upinzani mkali, Halmashauri ya Nchi iliripoti kwamba katika kipindi hicho, mikutano 31,488 ilifanywa nchini humo.

  • Urusi
    2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • “Mbali na familia yetu ni ndugu wachache sana waliojua kuhusu kazi ya kuchapisha. Kwa kuwa hakuna yeyote aliyekuwa akiniona nyakati za jioni, ndugu na dada kutanikoni walikuwa na hofu kuhusu hali yangu ya kiroho. Walikuwa wakija nyumbani kwangu kunitembelea ili kunitia moyo, lakini nyakati zote nilikuwa sipatikani. Ndiyo, nyakati hizo tulipokuwa tukichunguzwa sana, utendaji katika mahali pa kuchapishia ulikuwa wa siri sana.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki