-
Shabaha ya Mashambulizi ya SovietiAmkeni!—2001 | Aprili 22
-
-
Wasiwasi wao ulidhihirishwa wakati waliposhambulia Mashahidi mnamo mwezi wa Aprili 1951. Miaka miwili tu iliyopita, mnamo mwaka wa 1999, Profesa Sergei Ivanenko, msomi Mrusi anayeheshimiwa, alisema katika kitabu chake The People Who Are Never Without Their Bibles kwamba mapema mwezi wa Aprili 1951, “familia zaidi ya 5,000 za Mashahidi wa Yehova kutoka jamhuri za Sovieti za Ukrainia, Belorusia, Moldavia, na Baltiki zilihamishwa hadi ‘makao ya kudumu’ huko Siberia, Mashariki ya Mbali, na Kazakhstan.”
Tukio Linalostahili Kukumbukwa
Hebu wazia jitihada zilizohusika katika shambulizi hilo—kukusanya maelfu ya familia za Mashahidi kutoka kwenye eneo kubwa hivyo kwa siku moja tu? Wazia kukusanya mamia, ama maelfu ya watu, ili wafanye kazi ya kutambulisha Mashahidi, kisha kuvamia ghafula nyumba zao zote usiku mmoja. Halafu, kulikuwa na kazi ya kupakia watu kwenye mikokoteni, magari yanayokokotwa na wanyama, na magari mengine. Kisha kuwapeleka kwenye vituo vya magari ya moshi, na kuwapakia kwenye mabehewa ya mizigo.
Fikiria pia mateso yao. Je, waweza kuwazia pia jinsi walivyolazimishwa kusafiri kwa maelfu ya kilometa—kwa muda wa majuma matatu au zaidi, huku wakiwa kwenye mabehewa machafu, yaliyosongamana watu ambayo hayakuwa na vyoo ila ndoo ya kujisaidia tu? Jaribu kuwazia ukiachwa tu kwenye nyika ya Siberia. Nawe wafahamu kwamba si rahisi kuishi kwenye mazingira hayo magumu.
Mwezi huu ni ukumbusho wa miaka 50 tangu kuhamishwa kwa Mashahidi wa Yehova mnamo Aprili mwaka wa 1951. Masimulizi ya wale waliookoka ambayo yamerekodiwa kwenye ukanda wa vidio yanaonyesha jinsi walivyodumisha uaminifu licha ya kuteswa kwa miaka mingi. Masimulizi hayo yaonyesha kwamba jitihada za kuzuia watu kumwabudu Mungu haziwezi kufaulu. Hata Wakristo wa karne ya kwanza hawakuacha licha ya vizuizi.
Matokeo ya Uhamisho Huo
Serikali ya Sovieti iligundua upesi kwamba kuzuia Mashahidi kumwabudu Yehova hakukuwa kazi rahisi kama ilivyodhaniwa. Bila kujali malalamiko makali ya askari, Mashahidi walimwimbia Yehova sifa walipokuwa wakipelekwa uhamishoni. Waliangika ishara zilizosema hivi kwenye mabehewa yaliyowabeba: “Mashahidi wa Yehova Garini.” Shahidi mmoja alieleza hivi: “Tulipokuwa njiani tulikutana na magari mengine ya moshi vituoni, yaliyobeba wahamishwa, nasi tuliona ishara zilizoangikwa kwenye mabehewa.” Tulitiwa moyo kama nini!
Kwa hiyo badala ya kuvunjika moyo, wale waliokuwa wakihamishwa walidhihirisha roho kama ya mitume wa Yesu. Biblia yasema kwamba baada ya kupigwa viboko na kuagizwa wakome kuhubiri, ‘waliendelea bila kuacha kufundisha na kutangaza habari njema juu ya Kristo.’ (Matendo 5:40-42) Kwa kweli, ni kama Kolarz alivyosema kuhusu uhamisho huo, “haukuwa mwisho wa ‘Mashahidi’ nchini Urusi, ila ulikuwa mwanzo tu wa kazi yao ya kuwahubiria wengi. Hata walijaribu kuwahubiria watu vituoni wakiwa njiani kuelekea uhamishoni.”
Mashahidi walipowasili sehemu mbalimbali, walisifiwa kuwa wafanyakazi watiifu na wenye bidii. Lakini, kama mitume wa Kristo, ni kana kwamba waliwaambia wale waliowanyanyasa: ‘Hatuwezi kukoma kusema juu ya Mungu wetu.’ (Matendo 4:20) Wengi walisikiliza mafundisho ya Mashahidi na kujiunga nao kumtumikia Mungu.
Kolarz aeleza matokeo: “Serikali ya Sovieti ilipowahamisha ilisaidia sana kusambazwa kwa dini yao. ‘Mashahidi’ walihamishwa kutoka kwenye vijiji vyao vilivyojitenga [katika jamhuri za magharibi mwa Sovieti] na kupelekwa sehemu mbalimbali zenye watu wengi, kwenye kambi za mateso au za kazi ngumu.”
-
-
Shabaha ya Mashambulizi ya SovietiAmkeni!—2001 | Aprili 22
-
-
[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 7]
FAMILIA MOJA KATI YA MAELFU—Fyodor Kalin Asimulia Kuhamishwa kwa Familia Yao
Familia yetu iliishi katika kijiji cha Vilshanitsa, magharibi mwa Ukrainia. Alfajiri na mapema Aprili 8, 1951, maofisa waliokuwa na mbwa walikuja na kutuamsha sote. Walituambia kuwa serikali ya Moscow iliamuru tuhamishwe hadi Siberia. Lakini hatungehamishwa endapo tungetia sahihi hati iliyosema kwamba sisi si Mashahidi wa Yehova tena. Familia yetu yenye watu saba, wazazi wangu na ndugu zangu, tuliazimia kwamba hatutakana imani yetu. Nilikuwa na umri wa miaka 19 wakati huo.
Ofisa mmoja alisema hivi: “Bebeni maharagwe, mahindi, unga, vyakula vilivyohifadhiwa, na kabichi—la sivyo, watoto wenu watakula nini?” Tuliruhusiwa pia kuchinja kuku kadhaa na nguruwe na kubeba nyama hiyo. Vigari viwili vya kukokotwa na farasi vililetwa, na kila kitu kikapakiwa ndani yake na kupelekwa mji wa Hriplin. Huko tulijazwa kwenye behewa la mizigo watu 40 au 50 hivi, na mlango ukafungwa.
Behewa hilo lilikuwa na mbao chache za kulalia—hazikutosha kila mtu. Kulikuwa pia na jiko lenye makaa na kuni. Tulipika kwa jiko hilo, na kutumia vifaa vya kupikia tulivyobeba. Lakini hakukuwa na choo—tulitumia ndoo tu. Kisha tulitoboa shimo sakafuni, na kuitia ndoo shimoni, halafu tukaizingira kwa mablanketi kwa ajili ya faragha.
Tulisongamana sana kwenye behewa hilo na kusafiri polepole kwa maelfu ya kilometa na kuelekea tusikojua. Mwanzoni, tulivunjika moyo kidogo. Lakini tulipata shangwe tulipoimba pamoja nyimbo za Ufalme kwa shauku sana kiasi cha kupoteza sauti. Kamanda wa jeshi alifungua mlango na kutuamrisha tunyamaze, lakini hatukuacha kuimba hadi mwisho wa wimbo. Tuliposimama kwenye vituo njiani, wengi walikuja kujua kwamba ni Mashahidi wa Yehova waliokuwa wakihamishwa. Hatimaye, baada ya kusafiri kwa siku 17 au 18 tukiwa behewani, tulishushwa Siberia karibu na Ziwa Baikal.
[Picha]
Nimesimama mstari wa nyuma, kulia
-
-
Shabaha ya Mashambulizi ya SovietiAmkeni!—2001 | Aprili 22
-
-
[Picha katika ukurasa wa 6]
Maelfu walisafirishwa kwa mabehewa ya mizigo hadi Siberia
-
-
Jinsi Dini Ilivyookoka MashambuliziAmkeni!—2001 | Aprili 22
-
-
[Picha katika ukurasa wa 8, 9]
Vovchuk na mkewe walihamishwa hadi Irkutsk, Siberia, mwaka wa 1951 nao wangali Wakristo waaminifu leo
-