-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
Aleksey Gaburyak, aliyekuwa mwangalizi wa mzunguko kuanzia 1986 mpaka 1995, anakumbuka hivi: “Tulikutana na washiriki wa Halmashauri ya Nchi huko Usol’ye-Sibirskoye mwaka wa 1965. Ndugu hao walituomba tuwatafute ndugu na dada wote waliokuwa wametawanyika kwa sababu ya kuhamishwa, kufungwa gerezani, au kwa sababu ya mgawanyiko uliokuwepo na kuwaunganisha tena na makutaniko. Tulipewa anwani kadhaa. Eneo langu lilitia ndani wilaya ya Tomsk na Kemerovo na pia majiji ya Novokuznetsk na Novosibirsk. Ndugu wengine walipewa maeneo tofauti. Tulipaswa kupanga makutaniko na vikundi mbalimbali na pia kuwaweka rasmi na kuwazoeza ndugu wanaostahili. Isitoshe, tulihitaji kupanga jinsi ambavyo vichapo vingewafikia akina ndugu na kupanga mikutano ya kutaniko chini ya marufuku. Kwa muda mfupi tu, tulifanikiwa kuwatembelea ndugu na dada 84 ambao walikuwa wametenganishwa na tengenezo. Jinsi tulivyofurahi kuona kwamba ‘kondoo’ wa Yehova walisikia tena sauti ya Mchungaji Mwema na walimtumikia pamoja na watu wake!”—Yoh. 10:16.
-
-
Urusi2008 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
-
-
[Picha katika ukurasa wa 142]
Aleksey Gaburyak alisaidia kuwaunganisha wale waliokuwa wametawanyika
-