Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Estonia
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • “Kwa miaka mitano nilifanya kazi katika migodi ya makaa ya mawe,” asema Adolf Kose. “Tulikuwa kaskazini mwa Mzingo wa Aktiki, ambako wakati wa baridi kali, mwangaza wa jua hauonekani. Kulikuwa na giza wakati tulipotoka ndani ya mgodi baada ya kumaliza zamu yetu. Kwa hiyo, hatukuona mwangaza wa jua kwa miezi mingi. Pia, hatukupata chakula cha kutosha. Hali hiyo iliathiri kumbukumbu langu na uwezo wangu wa kukumbuka wakati. Kwa sababu ya kazi ngumu, ukosefu wa chakula, na uchovu mwingi, tulikuwa na nguvu kidogo tu za kuzungumza kwa dakika chache kuhusu mambo ya kawaida. Hata hivyo, tulipozungumzia kweli za Ufalme, hatukuhisi uchovu. Tungeendelea kwa muda mrefu.”

      Licha ya matatizo hayo yote, watu wa Yehova walijifunza kupendana bila ubinafsi. Ndugu Kose anaeleza, “Chochote tulichokuwa nacho au chochote ambacho mmoja wetu alipokea tulikigawa kwa usawa kati ya akina ndugu. Kila mmoja wetu alikuwa na uhitaji, kwa hiyo tulijifunza kugawana chochote tulichokuwa nacho.”—1 Yoh. 4:21.

  • Estonia
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • “Baadaye tulipelekwa kwenye kambi tofauti,” aeleza Ndugu Kose. “Ushahidi mkubwa ulikuwa ukitolewa katika kila chumba cha gereza. Wakati huo, niliweza kutoa ushahidi kwa njia kubwa zaidi ya vile nilivyoweza kufanya kabla ya kupelekwa kambini au tangu niachiliwe.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki