-
Kuhubiri Mahali Ambapo Ukristo Ulisitawi ZamaniMnara wa Mlinzi—2005 | Juni 15
-
-
Viziwi “Wanasikia” Habari Njema
Kuna zaidi ya viziwi 90,000 huko Italia. Katikati ya miaka ya 1970, Mashahidi walianza kufikiria kuwafundisha viziwi kweli za Biblia. Mwanzoni, baadhi ya Mashahidi ambao ni viziwi waliwafundisha Lugha ya Ishara ya Italia wahudumu wenzao waliokubali kusaidia watu walio na tatizo la kusikia. Halafu, viziwi wengi zaidi walianza kuonyesha kupendezwa na Biblia. Leo, zaidi ya watu 1,400 wanaotumia Lugha ya Ishara ya Italia wanahudhuria mikutano ya Kikristo. Makutaniko 15 na vikundi 52 vinafanya mikutano katika lugha hiyo ya ishara.
Mwanzoni, kuhubiria viziwi kulitegemea hasa mipango ya kila Shahidi. Lakini mwaka wa 1978, ofisi ya tawi ya Italia ya Mashahidi wa Yehova ilianza kupanga makusanyiko ya wilaya kwa ajili ya viziwi. Mnamo Mei mwaka huohuo, ilitangazwa kwamba kwenye kusanyiko la kimataifa lijalo huko Milan, kungekuwa na programu kwa ajili ya viziwi. Kusanyiko la kwanza la mzunguko kwa ajili ya viziwi lilifanywa kwenye Jumba la Kusanyiko huko Milan, mnamo Februari 1979.
Tangu wakati huo, ofisi ya tawi imetoa uangalifu mkubwa juu ya kuwalisha kiroho viziwi kwa kuwatia moyo wahubiri wengi waboreshe ustadi wao wa lugha ya ishara. Kuanzia mwaka wa 1995, mapainia wa pekee (waeneza-injili wa wakati wote) wametumwa katika vikundi kadhaa ili kuwazoeza Mashahidi ambao ni viziwi katika kuhubiri na kupanga mikutano ya Kikristo. Majumba matatu ya Kusanyiko yana video za kisasa ili kuwasaidia wahudhuriaji kutazama programu inapoendelea. Na kanda za video za vichapo vya Kikristo zinapatikana ili kuwalisha kiroho viziwi.
Watu wametambua kwamba Mashahidi wanahangaikia sana hali ya kiroho ya viziwi. Gazeti P@role & Segni linalotolewa na Shirika la Viziwi la Italia, lilinukuu barua moja iliyotumwa na askofu mmoja Mkatoliki ambayo ilisema hivi: “Kuwa kiziwi ni jambo lisilopendeza katika maana ya kwamba mtu ambaye ni kiziwi anahitaji uangalifu kila mara. Kwa mfano, anaweza kufika kanisani peke yake bila tatizo lolote, lakini anahitaji msaada wa mkalimani ili kufuata kila jambo linalosomwa, kusemwa, au kuimbwa wakati wa ibada.” Gazeti hilo linaongezea kusema kwamba, askofu huyo “anaeleza kuwa, kwa kusikitisha, kanisa halijajitayarisha kushughulikia tatizo hilo na kwamba watu wengi ambao ni viziwi wanashughulikiwa vizuri katika Majumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova kuliko katika makanisa.”
-
-
Kuhubiri Mahali Ambapo Ukristo Ulisitawi ZamaniMnara wa Mlinzi—2005 | Juni 15
-
-
kutaniko moja la Lugha ya Ishara ya Italia huko Roma
-